Jumanne, 20 Oktoba 2015

UMASKINI WA MALI AU UMASKINI WA FIKRA?

Inashangaza kuona watu wanambiwa na kupewa ahadi kuwa wataondolewa umaskini na kuwafanya wawe na maisha mazuri. Umaskini wanaouongelea waheshimiwa ni umaskini upi?kuna umaskini wa fikra, umaskini wa njaa, umaskini wa hela, na umaskini wa elimu,sasa waheshimiwa wakisimama kuwapigia watu tarumbeta ya kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini mbona hawaelezei namna na jinsi watakavyo mfanya kila mtanzania aondokane na umaskini wa aina zote zilizotajwa hapo juu?inawezekana ukawafanya watu wote nchi hii wakawa kweli matajiri au ni siasa inayosukuma hayo mambo kuliko utawala wa akili na kufikiri juu ya hao waheshimiwa wayasemayo?Hata nchi zilizoendelea bado zina maskini,inakuwaje sisi Leo tuambiwe kuwa baada ya uchaguzi tunakuwa matajiri bila hata ya kuonyeshwa ishara halisi kimatendo ila kwa maneno ndo kwingi?Hayo yote ni kuongelea mdomoni kuliko kongelea akilini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni