Jumanne, 20 Oktoba 2015

JIBADILISHE KABLA HUJABADIRISHWA

Itawezekana kupata mabadiliko ikiwa wanaodai hayo mabadiliko hata wao wenyewe hawajajiletea mabadiliko hata kwa mambo madogo waliyonayo?mfano kama mtu anadai mabadiliko wakati hata magugu yaliyozunguka nyumba yake yanamshinda kuyangoa, mtu akishindwa kufagia nyumba yake na kuipanga vizuri na hata akashindwa kupanga chumba chake anapolala mwenyewe sasa ukisikia huyo anadai mabadiliko huyo kweli anadai mabadiliko kutoka ndani ya moyo wake au ni msukumo wa mikumbo ili mradi siku imeenda?Itawezekana kweli kudai mabadiliko ihali mdai mabadiliko hajajibadilisha na kubadilika na hatimaye kudai ili abadilishwe zaidi.Kamwe haitowezekana mabadiliko kwa watu kama watu wenyewe hawajajibadilisha katika vitu vifuatavyo:1.Kujibadilisha kifkra 2.Kujibadilisha kimtizamo hasa juu ya kufikiri,kutenda, na kuchukulia uhalisia wa mambo.3.Kujenga mtizamo chanya na kujikubali mapungufu 4.Kuondoa dhana ya kujihisi wanyonge daima na hivyo kujenga dhana ya kuwa wategemezi daima. Kwa hili ni kuwa dhana ya kutegemea kila kitu kupewa ndo wengi tumejikuta tunaitwa mbumbumbu na hivyo kutengeneza mwanya kwa waheshimiwa kutoa ahadi hewa za mabadiliko yasiyokuwepo.Tusipojibadili namna ya kuchukulia na kufanya mambo tutajikuta hatuna mabadiliko kamwe.Haiwezekani ukalala bila ya kufanya lolote na hapo ukategemea mabadiliko yatokee.Kuleta mabadiliko ni moja ya mapinduzi katika historia.Tukumbuke kuwa hustoria ni kwa wale tu waitengenezayo(history is only for those who make it,never sleep and expect history to be made for you).Mabadiliko yatakuja pale ambapo tulisha anza sisi wenyewe kwa Yale madogo tuliyoanzisha kwa juhudi zetu wenyewe

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni