Inashangaza kuona watu wanambiwa na kupewa ahadi kuwa wataondolewa
umaskini na kuwafanya wawe na maisha mazuri. Umaskini wanaouongelea
waheshimiwa ni umaskini upi?kuna umaskini wa fikra, umaskini wa njaa,
umaskini wa hela, na umaskini wa elimu,sasa waheshimiwa wakisimama
kuwapigia watu tarumbeta ya kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini mbona
hawaelezei namna na jinsi watakavyo mfanya kila mtanzania aondokane na
umaskini wa aina zote zilizotajwa hapo juu?inawezekana ukawafanya
watu wote nchi hii wakawa kweli matajiri au ni siasa inayosukuma hayo
mambo kuliko utawala wa akili na kufikiri juu ya hao waheshimiwa
wayasemayo?Hata nchi zilizoendelea bado zina maskini,inakuwaje sisi Leo
tuambiwe kuwa baada ya uchaguzi tunakuwa matajiri bila hata ya
kuonyeshwa ishara halisi kimatendo ila kwa maneno ndo kwingi?Hayo yote
ni kuongelea mdomoni kuliko kongelea akilini.
Jumanne, 20 Oktoba 2015
UMRI WA UZEE NA MAHITAJI YAKE
Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee
anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo
asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba
au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na
hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na
wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu
kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama
msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa
mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe
pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi
wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto
ELIMU NA UMUHIMU WAKE
Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu
mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana
na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa
uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika
mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji
waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke
kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi
mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya
kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi
weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa
nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia
ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao
walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai
wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert
na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na
kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia
zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora
za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu
wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao
hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi
wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa
mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila
mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi
akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana
ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao
JIBADILISHE KABLA HUJABADIRISHWA
Itawezekana kupata mabadiliko ikiwa wanaodai hayo mabadiliko hata wao
wenyewe hawajajiletea mabadiliko hata kwa mambo madogo waliyonayo?mfano
kama mtu anadai mabadiliko wakati hata magugu yaliyozunguka nyumba yake
yanamshinda kuyangoa, mtu akishindwa kufagia nyumba yake na kuipanga
vizuri na hata akashindwa kupanga chumba chake anapolala mwenyewe sasa
ukisikia huyo anadai mabadiliko huyo kweli anadai mabadiliko kutoka
ndani ya moyo wake au ni msukumo wa mikumbo ili mradi siku
imeenda?Itawezekana kweli kudai mabadiliko ihali mdai mabadiliko
hajajibadilisha na kubadilika na hatimaye kudai ili abadilishwe
zaidi.Kamwe haitowezekana mabadiliko kwa watu kama watu wenyewe
hawajajibadilisha katika vitu vifuatavyo:1.Kujibadilisha kifkra
2.Kujibadilisha kimtizamo hasa juu ya kufikiri,kutenda, na kuchukulia
uhalisia wa mambo.3.Kujenga mtizamo chanya na kujikubali mapungufu
4.Kuondoa dhana ya kujihisi wanyonge daima na hivyo kujenga dhana ya
kuwa wategemezi daima. Kwa hili ni kuwa dhana ya kutegemea kila kitu
kupewa ndo wengi tumejikuta tunaitwa mbumbumbu na hivyo kutengeneza
mwanya kwa waheshimiwa kutoa ahadi hewa za mabadiliko
yasiyokuwepo.Tusipojibadili namna ya kuchukulia na kufanya mambo
tutajikuta hatuna mabadiliko kamwe.Haiwezekani ukalala bila ya kufanya
lolote na hapo ukategemea mabadiliko yatokee.Kuleta mabadiliko ni moja
ya mapinduzi katika historia.Tukumbuke kuwa hustoria ni kwa wale tu
waitengenezayo(history is only for those who make it,never sleep and
expect history to be made for you).Mabadiliko yatakuja pale ambapo
tulisha anza sisi wenyewe kwa Yale madogo tuliyoanzisha kwa juhudi zetu
wenyewe
LUGHA NA MATUMIZI YAKE
Matumizi ya lugha isivyo hitajika yaweza kupoteza ukweli wa mambo
kihalisia na kufanya hata watu wasiohusika hata vitu visivyoweza kutumia
ufahamu(reasoning) kuonekana kuwa vina hatia. Mara nyingi tumeshuhudia
mfano ajali nyingi hapa kwetu na duniani kote.Ajali kama hizo
zimehusisha watu kupoteza maisha kutokana na hizo ajali. Mfano
tumeshuhudia ajali za vyombo vya moto kama vile pikipiki na magari,
ndege,na vinginevyo. Jambo ambalo huwa daima linanishangazaga ni kwenye
mawasiliano wakati wa kutoa taarifa
baada ya kutokea ajali mfano utasikia mtu anaongea kuwa " nimeangushwa
na pikipiki,au nimeangushwa na gari" hivi kweli hii inawezekana
kimaongezi kuwa mtu ameangushwa na pikipiki au gari? mimi naona kuwa
hiyo siyo sahihi kamwe.Daima mtu huwa ndo anaiangusha pikipiki au gari
maana hivi vifaa vya usafiri huwa havina akili au utashi wa kuamua
kumdondosha mtu bali uzembe wa mtu huwa ndo unamfanya adondoshwe au
aangushwe na hicho kifaa cha usafiri.Hiyo ndo kawaida yetu binadamu kuwa
huwa hatupendi kuwajibika kutokana na uzembe wetu baadala yake ni
kuhamishia maumivu na hisia kwa watu na hata vitu visivyo na uhai
kuhusika na mikosi tuipatayo. Nimesikia mara nyingi mtu mmoja akisema
kuwa kamwe hatopanda pikipiki, nilipomuuliza sababu ya kusema vile
akaniambia kuwa ni kwa kuwa pikipiki zimeangusha na kuua watu
wengi;swali langu kwake lilibaki kuwa " je pikipiki huwa inaangusha mtu
au mtu huwa ndo anaiangusha?" Uwajibikaji ni muhimu kabla ya kuelekeza
tuhuma kwa wengine.
KWA NINI WALIMU WANAPATA UJIRA WA KUBABAISHA?
Tujiulize swali la msingi kuwa kama walimu wetu wangelikuwa wanalipwa
posho kama za wabunge kwa mwezi kungelitokea nini katika sekta ya
elimu?Hivi huyu anayeenda kuwakilisha wananchi katika chombo cha dola
ambacho ni moja ya mihili mikuu ya serikali kimaarifa au kielimu huyu
inasemwa kuwa walau awe na elimu ya kidato cha nne na zaidi ajue kusoma
na kuandika basi. Cha kushangaza na kuchekesha ni kuwa huyu ambaye
anasemwa kuwa ajue kusoma na kuandika mara nyingi huwa tunawaona kupitia
Luninga wakiwa wamechapa usingizi na kusahau kile kilichowafanya wawe
hapo;kisa ni kujua kusoma na kuandika na mwishowe huyo anapata posho
Mara nne au tano ya mwalimu au mtu yeyote mtaaluma ambaye kila siku
lazima asumbue kichwa chake kufanya kazi Fulani,wakati waheshimiwa
wanalala na posho inaingia.Hivi ninani ambaye hawezi simama pale bungeni
na kutoa hoja? kusimama pale kunahitaji kuumiza vichwa kweli?jibu ni
hapana ila kukaa pale ni sawa na kusema kama waswahili wa mtaani
wasemavyo"kula kuku kwa mrija." Hii itakuwa sahihi nikisema kuwa baadhi
ya wataaluma wetu hasa maprofessa wetu wa vyuo vikuu wanaacha fani zao
na kukimbilia kwenye siasa maana huko kuna ulaji kwa njia ya mtelemko
bila ya kusumbua vichwa.Hivi kama hao wanaokimbia fani zao na kuingia
katika siasa wangelikuwa wanapewa keki wanayopewa hawa waheshimiwa
bungeni tungelikuwa hatua ya juu sana kielimu. Uwezo wa kujenga hoja na
fikra hautegemei kusoma na kuandika,Bali unahitaji pia nguvu ya
kufikiria na kujenga hoja makini.Wale waliopaswa kushauri wanaoongoza
pia nao wanataka kuongoza,je hapo nani atatoa maoni na ushauri kwa
wanaoongoza?matokeo yake ni kuishia katika ushabiki usiojenga
MAADILI JUU YA AHADI.
Ahadi yaweza kuleta matumaini ya kuishi kwa muda mrefu bila ya kuona
ukweli wenyewe au uhalisia wa hiyo ahadi.Kwa kifupi naweza sema ahadi
siyo tofauti na ndoto maana hivyo vyote ni ishara zinazolenga kwenye
uhalisia japo zenyewe siyo uhalisia(reality)kamwe. Ahadi ni kama vile
mtu kusikia harufu ya chakula kikipikwa au kukaangwa akasikia kushiba
kumbe ihali bado ana njaa ya kutosha. Sasa wengi wetu ndo hali
tuliyoifikia wakati tukielekea uchaguzi mkuu.Hivi hizi ahadi
zinazotolewa na waheshimiwa tukapiga makofi kwa nguvu tukafanana na
waliokwisha kula na kushiba, hivi huu ni ukweli na uhalisia au bado tuko
kwenye ndoto?.Kuna namna nyingi zakudanganywa na ukakubali kiulaini
bila ya manunguniko.Njia mojawapo ni ahadi ambazo ni nusu ya uhalisia na
nusu uongo.
KWA NINI KUTAWALIWA NA HISIA BAADALA YA KUTAWALIWA NA UFAHAMU?
Ni jambo la kushangaza kuona watu wanatawaliwa na hisia(feelings) za
wengine na kuzifanya hisia zao.Kimsingi kundi la watu wa namna hiyo
linakuwa limepoteza malengo na mwelekeo kwa ujumla katika
maisha.Ukiangalia ushabiki unaofanywa kwa sasa katika vyama vya siasa
unaweza tambua kuwa sio mashabiki wote wanajua walitendalo ila wengi wao
huenda kwa mkumbo wa kwa kuwa Fulani kashabikia hebu na Mimi nishabikie
kitu ambacho ni hatari katika maendeleo na utu wa kila mmoja wetu.Hivyo
hatuko mbali kusema kuwa ushabiki ninamna ya watu kuishi maisha ya
wengine ili mradi siku ipite.Ushabiki lazima uwe na tija na malengo pia
ya kumnufaisha mwananchi kuliko kumnufaisha mgombea.Ni heri kutoshabikia
yale tusiyoyajua maana wanaofaidika ni wengine.Kwa jina la ushabiki
wengine wameshanunuliwa kwa kilauri/kiloba wakiwa wamesahau kuwa wanauza
utu wao na haki zao kwa vitu vya mpito visivyokumbukwa daima.
NANI AHUDUMIWE NA NANI ALALAMIKIWE?
Kama wanaohudumiwa wanawalaumu na kuwalalamikia sana wanaowahudumia, je
wanaohudumia watahudumiwa na nani?na wakilalamikiwa nawao watamlalamikia
nani? Siyo vema kulaumu na kulalamika kilawakati maana na hao
wanaolalamikiwa wana haki ya kulalamika nao ni binadamu kama binadamu
wengine.
MIFUMO NA MADHARA YAKE
Kuna wengi ambao kiutendaji huonekana wema.Tatizo linakuja pale ambapo
utendaji wao unazoroteshwa na kumezwa na mfumo mama uliowalea hadi
wakaota vitambi na mvi.Hao watendaji daima huishia kuumia na kuzikana
nafsi zao ili waendelee kulea na kubeza mifumo iliyowalea hata kama
wanaona kuna mapungufu.Wakijaribu kuinua na kupaza sauti zao wanajikuta
wanalaumiwa na kulumbambana na hao wazazi wao(mifumo)iliyowalea.Mifumo
ipo na inaendelea kuwepo katika jamii ili iendelee kuneemeka.Waendao
tofauti na mifumo hao ndo wanaonekana kukimbilia upande mwingine wa
shilingi. Pia ikumbukwe kuwa mifumo imetawala nyanja mbalimbali mbali
katika jamii yetu. Wale ambao wanaonekana wema na watakatifu na
wanaopaza sauti zao wakilalamikia mifumo iliyopo kwa sasa, wakishapewa
nyenzo tutashuhudia mda si mrefu wao watajenga mifumo ya namna
gani?either mfumo wa kujifaidisha wenyewe au mfumo kwa ajili ya manufaa
ya wote?lazima tutambue kuwa binadamu ni fumbo ambalo halijafumbuliwa na
lisilo rahisi kueleweka kwa kila mtu.Yule anayelia na kuwafanya wengine
walie,je wale waliao wakimfikisha mliaji anapotaka je wao wakianza
kulia atawasindikiza na kuwafikisha wanapotaka(wananchi)?Wanaoonekana
kuomboleza wakisha fikishwa mahala pao wanapotaka daima hujenga kuta ili
kuwazuia waombolezaji wasiingie pale walipofika(Ikulu).Tusikumbwe daima
na mikumbo ya kutekwa na kuwa watumwa wa mifumo tusiyo ijua malengo
yake.
UCHAGUZI MKUU UMETUFIKIRISHA NINI?
Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo
kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo
kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao
waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga
ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi
watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu
mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani
alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama
chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika
chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au
watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa
wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake,
kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni
mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona
wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo
kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa
watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama
ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi
waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita
kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha
kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika
kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa
kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of
generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na
baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.
MCHEZO WA SIASA NI MCHEZO WA NAMNA GANI?
Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo
kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo
kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao
waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga
ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi
watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu
mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani
alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama
chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika
chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au
watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa
wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake,
kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni
mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona
wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo
kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa
watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama
ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi
waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita
kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha
kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika
kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa
kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of
generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na
baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.
HUU NI WENDAWAZIMU KUPIGA BARABARA DEKI AU?
Nijambo la kutafakarisha kuona watu wanapiga barabara deki tena kwa
nguvu zote! na hili kimsingi siyo jambo la kawaida hata kidogo.Waweza
jiuliza nini kinawasukuma watu kufanya hivyo?je wanafanya hivyo kwa
ushabiki au kufanya hivyo kunaashiria jambo Fulani? Kama tujuavyo watu
wakifanya hivyo wanakuwa wanaashiria jambo fulani kwa kutarajia litokee
na kuwafanya wawe katika hali fulani ya maisha. Tunajua kabisa kuwa
alama zionyeshapo uendapo huwa daima zinasaidia kuonyesha mahali
sahihi unapohitaji kwenda japo alama zenyewe siyo mahali unapotaka
kwenda. Tukiona watu wanapiga deki na kupangusa Barabara wanakuwa hasa
wanatoa ishara gani? hapo twaweza kuwa na majibu na fikra nyingi.
Mojawapo ikiwa ni kwamba wamechoshwa na mfumo mbovu wa uongozi wanataka
uongozi mpya na dira mpya ya maendeleo, au kwamba wananchi wanataka sasa
kupumulia mahala pazuri pasipo hila wala uyanganyi wala ufisadi n.k
hayo ni baadhi ya majibu waliyonayo wapiga kura.Kiuhalisia siyo jambo la
kufikirika watu kutumia mda wao mwingi kusafisha barabara pasipo
kuambiwa kufanya hivyo au pasipo malipo isipokuwa kuna jambo fulani
ambalo kwa wasio funguka macho bado ni kitendawili.
MTU NA UTU WAKE
Ukitaka kutambua utu wa mtu na kumjua yeye ninani mpe Uhuru wa umfanyie
nini?hapo ni dhahiri kuwa utapata majibu mengi kutoka kwa huyo mtu juu
ya analotaka umfanyie hata kama mengine yapo juu ya uwezo wake.Katika
nafasi hiyo utapata kutambua kama huyo mtu ni mchoyo na pia mwenye uchu
wa kutaka kutawala au pia utapata kujua unyenyekevu wa huyo mtu kadiri
ya kitu ambacho amekuomba ukamfanyie.Sasa tuje ngambo nyingine ya
Shilingi ambapo Leo hii tumeshuhudia wale waliokuja kutuomba
dhamana ya kuongoza nchi.Wao wakati wanahangaika ili tuwape dhamana ya
kutuongoza mambo yamekuwa kama ifuatavyo:1.Wao wamekuja na bado wanazidi
kuja kwetu na tumewauliza "je mwataka tuwafanyie nini?" Wao wakajibu
kwa sauti kubwa "mtupigie kura ya ndiyo katika uchaguzi mkuu
ujao."2.Pindi na sisi ilipokuwa zamu yetu juu ya wao watufanyie nini,
wamekuja na majibu mbalimbali yenye kutia moyo japo hayana uhakika
asilimia mia moja.Moja ya majibu mepesimepesi ni kufuta baadhi ya Kodi,
Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.Kuanzisha viwanda,
kuhakikisha kuwa vijana wote(waliosoma na wasiosoma)wanapata ajira na
wanakuwa na maisha mazuri n.k.Hayo yote ni mazuri sana ila wengi wetu
tunasahau kuwa siyo kila ahadi utekelezeka! Kwa Mawazo yangu ni kuwa
itakuwa rahisi kwetu kutoa majibu ya maswali yetu ya tuwafanyie nini
waheshimiwa maana majibu yanaeleweka, kuwa tutawapigia kura ya
ndiyo.Wasiwasi unakuja kwa majibu ya maswali yetu kwao kuwa watatufanyia
nini?majibu yao kwetu yamekuja na ahadi ambazo ni vigumu kuamini kuwa
zitatekelezeka.Tunasahau kuwa Siasa ni mchezo ambao siyo wote twaweza
kuucheza. Punde tutashuhudia kama tulidanganywa juu ya hizo ahadi au la!
wakishapewa hayo majukumu ndoo itakuwa kutekeleza au kutokuteleza hizo
ahadi.Hofu yangu ni kwamba kwa nchi kama Tanzania,Ahadi zilizotolewa
baadhi ziko nje ya uwezo wake, kama vile Elimu bure na ajira kwa kila
mtanzania hasa vijana.Hayo yote ni majibu ya tutafanyiwa nini.Yatubidi
tufunguke macho na kuelewa kati ya kuambiwa ukweli au kulaghaiwa.
LUGHA YA BAO LA MKONO
Kwa sasa tunaambiwa lugha ya bao la mkono! bao la mkono halikulezewa
vizuri na kuzungumzika vizuri.Mtoa hoja angelielezea vizuri ni mchezo
gani ambapo bao la mkono ni marufuku mfano katika kucheza mpira wa miguu
ukifunga bao la mkono jua kuwa kuna adhabu juu yake(Penalty) wakati
kama unacheza Mpira wa mikono(volleyball au Basketball) gori la mkono
hapo hapo halina shida. Shida ni pale bao la mkono linafungwa wakati wa
mchezo wa mpira wa kutumia miguu.Afungaye kutumia mkono kwa
mchezo wa Mpira wa miguu hapo inamhitaji abadilike. Katika mfumo wetu
wa utawala yaonekana wananchi wameumizwa vibaya na kufikiria vinginevyo
kwamba mabao yanayofungwa siyo halali kwa kuwa mchezo unaochezwa ni
mchezo wa mpira wa miguu lakini bado mabao yanayofungwa ni ya mkono
pasipo halali(utumiaji wa nguvu kupita kiasi na rushwa).Bao la mkono
litatambulika kuwa hivyo na halali pindi mchezo ukiwa wa kuchezwa kwa
mikono na siyo miguu.Kama wananchi wanalalamikia bao la mkono hii
inamaana gani? kwamba mchezo unaochezwa ni wa miguu ambao kiutaratibu
lazima bao kama bao linafungwa kwa miguu,Ila matokeo yake washangiliaji
wanaona bao linafungwa kwa mkono wanashangaa na kufikiri kutowezekana
kwa hilo bao lililofungwa na wakati huo refaree anaweka tiki kuwa ni bao
stahiki mbali ya kujuakuwa siyo halali.Tujiulize kuwa katika uwanja wa
Siasa wachezaji wanacheza mchezo gani? wa kukubali mshindi halali au
lile bao la mkono?
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)