Kuna wengi ambao kiutendaji huonekana wema.Tatizo linakuja pale ambapo
utendaji wao unazoroteshwa na kumezwa na mfumo mama uliowalea hadi
wakaota vitambi na mvi.Hao watendaji daima huishia kuumia na kuzikana
nafsi zao ili waendelee kulea na kubeza mifumo iliyowalea hata kama
wanaona kuna mapungufu.Wakijaribu kuinua na kupaza sauti zao wanajikuta
wanalaumiwa na kulumbambana na hao wazazi wao(mifumo)iliyowalea.Mifumo
ipo na inaendelea kuwepo katika jamii ili iendelee kuneemeka.Waendao
tofauti na mifumo hao ndo wanaonekana kukimbilia upande mwingine wa
shilingi. Pia ikumbukwe kuwa mifumo imetawala nyanja mbalimbali mbali
katika jamii yetu. Wale ambao wanaonekana wema na watakatifu na
wanaopaza sauti zao wakilalamikia mifumo iliyopo kwa sasa, wakishapewa
nyenzo tutashuhudia mda si mrefu wao watajenga mifumo ya namna
gani?either mfumo wa kujifaidisha wenyewe au mfumo kwa ajili ya manufaa
ya wote?lazima tutambue kuwa binadamu ni fumbo ambalo halijafumbuliwa na
lisilo rahisi kueleweka kwa kila mtu.Yule anayelia na kuwafanya wengine
walie,je wale waliao wakimfikisha mliaji anapotaka je wao wakianza
kulia atawasindikiza na kuwafikisha wanapotaka(wananchi)?Wanaoonekana
kuomboleza wakisha fikishwa mahala pao wanapotaka daima hujenga kuta ili
kuwazuia waombolezaji wasiingie pale walipofika(Ikulu).Tusikumbwe daima
na mikumbo ya kutekwa na kuwa watumwa wa mifumo tusiyo ijua malengo
yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni