Jumanne, 20 Oktoba 2015

MIFUMO NA MADHARA YAKE

Kuna wengi ambao kiutendaji huonekana wema.Tatizo linakuja pale ambapo utendaji wao unazoroteshwa na kumezwa na mfumo mama uliowalea hadi wakaota vitambi na mvi.Hao watendaji daima huishia kuumia na kuzikana nafsi zao ili waendelee kulea na kubeza mifumo iliyowalea hata kama wanaona kuna mapungufu.Wakijaribu kuinua na kupaza sauti zao wanajikuta wanalaumiwa na kulumbambana na hao wazazi wao(mifumo)iliyowalea.Mifumo ipo na inaendelea kuwepo katika jamii ili iendelee kuneemeka.Waendao tofauti na mifumo hao ndo wanaonekana kukimbilia upande mwingine wa shilingi. Pia ikumbukwe kuwa mifumo imetawala nyanja mbalimbali mbali katika jamii yetu. Wale ambao wanaonekana wema na watakatifu na wanaopaza sauti zao wakilalamikia mifumo iliyopo kwa sasa, wakishapewa nyenzo tutashuhudia mda si mrefu wao watajenga mifumo ya namna gani?either mfumo wa kujifaidisha wenyewe au mfumo kwa ajili ya manufaa ya wote?lazima tutambue kuwa binadamu ni fumbo ambalo halijafumbuliwa na lisilo rahisi kueleweka kwa kila mtu.Yule anayelia na kuwafanya wengine walie,je wale waliao wakimfikisha mliaji anapotaka je wao wakianza kulia atawasindikiza na kuwafikisha wanapotaka(wananchi)?Wanaoonekana kuomboleza wakisha fikishwa mahala pao wanapotaka daima hujenga kuta ili kuwazuia waombolezaji wasiingie pale walipofika(Ikulu).Tusikumbwe daima na mikumbo ya kutekwa na kuwa watumwa wa mifumo tusiyo ijua malengo yake.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni