Kwa sasa tunaambiwa lugha ya bao la mkono! bao la mkono halikulezewa
vizuri na kuzungumzika vizuri.Mtoa hoja angelielezea vizuri ni mchezo
gani ambapo bao la mkono ni marufuku mfano katika kucheza mpira wa miguu
ukifunga bao la mkono jua kuwa kuna adhabu juu yake(Penalty) wakati
kama unacheza Mpira wa mikono(volleyball au Basketball) gori la mkono
hapo hapo halina shida. Shida ni pale bao la mkono linafungwa wakati wa
mchezo wa mpira wa kutumia miguu.Afungaye kutumia mkono kwa
mchezo wa Mpira wa miguu hapo inamhitaji abadilike. Katika mfumo wetu
wa utawala yaonekana wananchi wameumizwa vibaya na kufikiria vinginevyo
kwamba mabao yanayofungwa siyo halali kwa kuwa mchezo unaochezwa ni
mchezo wa mpira wa miguu lakini bado mabao yanayofungwa ni ya mkono
pasipo halali(utumiaji wa nguvu kupita kiasi na rushwa).Bao la mkono
litatambulika kuwa hivyo na halali pindi mchezo ukiwa wa kuchezwa kwa
mikono na siyo miguu.Kama wananchi wanalalamikia bao la mkono hii
inamaana gani? kwamba mchezo unaochezwa ni wa miguu ambao kiutaratibu
lazima bao kama bao linafungwa kwa miguu,Ila matokeo yake washangiliaji
wanaona bao linafungwa kwa mkono wanashangaa na kufikiri kutowezekana
kwa hilo bao lililofungwa na wakati huo refaree anaweka tiki kuwa ni bao
stahiki mbali ya kujuakuwa siyo halali.Tujiulize kuwa katika uwanja wa
Siasa wachezaji wanacheza mchezo gani? wa kukubali mshindi halali au
lile bao la mkono?
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni