Jumanne, 20 Oktoba 2015

LUGHA YA BAO LA MKONO

Kwa sasa tunaambiwa lugha ya bao la mkono! bao la mkono halikulezewa vizuri na kuzungumzika vizuri.Mtoa hoja angelielezea vizuri ni mchezo gani ambapo bao la mkono ni marufuku mfano katika kucheza mpira wa miguu ukifunga bao la mkono jua kuwa kuna adhabu juu yake(Penalty) wakati kama unacheza Mpira wa mikono(volleyball au Basketball) gori la mkono hapo hapo halina shida. Shida ni pale bao la mkono linafungwa wakati wa mchezo wa mpira wa kutumia miguu.Afungaye kutumia mkono kwa mchezo wa Mpira wa miguu hapo inamhitaji abadilike. Katika mfumo wetu wa utawala yaonekana wananchi wameumizwa vibaya na kufikiria vinginevyo kwamba mabao yanayofungwa siyo halali kwa kuwa mchezo unaochezwa ni mchezo wa mpira wa miguu lakini bado mabao yanayofungwa ni ya mkono pasipo halali(utumiaji wa nguvu kupita kiasi na rushwa).Bao la mkono litatambulika kuwa hivyo na halali pindi mchezo ukiwa wa kuchezwa kwa mikono na siyo miguu.Kama wananchi wanalalamikia bao la mkono hii inamaana gani? kwamba mchezo unaochezwa ni wa miguu ambao kiutaratibu lazima bao kama bao linafungwa kwa miguu,Ila matokeo yake washangiliaji wanaona bao linafungwa kwa mkono wanashangaa na kufikiri kutowezekana kwa hilo bao lililofungwa na wakati huo refaree anaweka tiki kuwa ni bao stahiki mbali ya kujuakuwa siyo halali.Tujiulize kuwa katika uwanja wa Siasa wachezaji wanacheza mchezo gani? wa kukubali mshindi halali au lile bao la mkono?

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni