Jumanne, 11 Aprili 2017

UKIKUTANA NA CHANGAMOTO MSHUKURU MUNGU, MAANA NI NDANI YA HIZO CHANGAMOTO UNAPATA FURSA ZA KUVUMBUA SULUHISHO LA HAYO MATATIZO

Watu katika ajira ziwe ni ajira za serikali au ajira za mashirika binafsi yasiyo ya serikali huwa daima katika utendaji wao huwa wanapata kuhamishwa kutoka kituo kimoja cha kazi kwenda kituo kingine cha kazi na wakuu wao wa idara. Katika kuhamishwa kwa mfanyakazi kutoka kituo kimoja kwenda kingine huwa daima sababu zifuatazo zinapelekeaga kuhamishwa kwa mfanyakazi Fulani:
1.Amehamishwa kwa kuwa ameonekana kuwa mtendaji mzuri hivyo aende akatende vivyohivyo katika eneo kingine... ambalo halina mtendaji mwingine mzuri kama huyo.
2.Ni mtendaji mbaya, ni mzembe, hivyo hilo eneo alipo hafai kufanya kazi aliyopewa, kwa maana kwamba huyo hasipohamishwa ataendelea kuharibu kazi ya serikali au kampuni, ni kwa msingi huo uhamisho wa namna hii huambatana na kubadilishiwa kazi baadala ya kuendelea na kazi hiyo hiyo.

3. Uhamisho ambao matokeo yake ni mgogoro/kutohelewana kati ya mwajiri/kiongozi wa idara na mwajiliwa. Daima mwajiri/kiongozi wa idara akiona kuwa mwajiriwa wake anakuwa mwerevu kumpita au hawaelewani kwa mambo Fulani kati yao, mwajili kwake hufanya kitu kidogo ili kuondoa huo mwiba ulio nyayoni mwake(mwajiriwa) Afanyacho kiongozi huyo ni kumpa uhamisho huyo mwajiliwa kwa kumpeleka maeneo ambayo huyo mwajiliwa hatoridhishwa nayo na hivyo anaweza acha hiyo kazi(akufukuzaye hakwambii toka).
Kwangu ni kwa hiyo namba tatu, kwamba kama anayehamishwa anapewa uhamisho kama adhabu, hana budi kufurahi na kushangilia maana anavyohamishwa kupelekwa mazingira magumu/hatarishi ndoo vivyo hivyo atatumia akili yake, uweza wake, na ujuzi wake kujifunza namna ya kupambana na hali ngumu. Tena faida kwa huyo ni kwamba aweza kuwa na ujuzi zaidi hata kumpita yule aliyemwamisha kituo cha kazi. Daima ukihamishwa mshukuru aliyekuhamisha hata kama ilikuwa kwa lengo baya,maana kwa jinsi hiyo anakuongezea weredi wa kufikiri na kuwa na ujuzi mpya katika kuona mazingira hatarishi kama moja ya fursa za kukusaidia kutenda vyema na kujifunza zaidi kutoka katika mazingira yaonekanayo hatarishi kwake.

NDANI YA GIZA HUWA NDOO TUNAPATAGA SULUHISHO LA KUTENGENEZA MWANGA

Ukipata kuona kuwa giza limetawala sana bila ya kukucha, basi fungua dirisha la imani yako na tafakari haya: Nyota huonekana vyema katika usiku wa kiza. Vivyo hivyo ni ndani ya dimbwi la matatizo huwa ndoo tunapata fursa za uvumbuzi, kujifunza na kutatua matatizo.

MATUMIZI MABAYA YA SILAHA ZA MOTO

    Tanzania kumekuwepo utaratibu wa kupewa kitambulisho kwa kila raia.
    Lakini cha ajabu nimeona katika habari mmoja alivyoulizwa atoe kitambulisho chake, akatoa bastola! Kumbe hizo bastola ndoo vitambulisho vipya vilivyoidhinishwa?

BINADAMU DAIMA HAKOSAGI KISINGIZIO

    Apambanaye ili ale keki akaikosa daima huishia kulaumu kuwa keki ni chanzo cha ugonjwa wa sukari, hivyo huishia kula viazi kama mbadala, ila akiitiwa ale hiyo keki hutupa viazi pembeni na kukimbilia hiyo keki aliyoituhumu hapo kabla kuwa ni chanzo cha ugonjwa wa sukari.

Jumanne, 20 Oktoba 2015

UMASKINI WA MALI AU UMASKINI WA FIKRA?

Inashangaza kuona watu wanambiwa na kupewa ahadi kuwa wataondolewa umaskini na kuwafanya wawe na maisha mazuri. Umaskini wanaouongelea waheshimiwa ni umaskini upi?kuna umaskini wa fikra, umaskini wa njaa, umaskini wa hela, na umaskini wa elimu,sasa waheshimiwa wakisimama kuwapigia watu tarumbeta ya kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini mbona hawaelezei namna na jinsi watakavyo mfanya kila mtanzania aondokane na umaskini wa aina zote zilizotajwa hapo juu?inawezekana ukawafanya watu wote nchi hii wakawa kweli matajiri au ni siasa inayosukuma hayo mambo kuliko utawala wa akili na kufikiri juu ya hao waheshimiwa wayasemayo?Hata nchi zilizoendelea bado zina maskini,inakuwaje sisi Leo tuambiwe kuwa baada ya uchaguzi tunakuwa matajiri bila hata ya kuonyeshwa ishara halisi kimatendo ila kwa maneno ndo kwingi?Hayo yote ni kuongelea mdomoni kuliko kongelea akilini.

UMRI WA UZEE NA MAHITAJI YAKE

Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto

ELIMU NA UMUHIMU WAKE

Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao