Watu katika ajira ziwe ni ajira za serikali au ajira za mashirika binafsi yasiyo ya serikali huwa daima katika utendaji wao huwa wanapata kuhamishwa kutoka kituo kimoja cha kazi kwenda kituo kingine cha kazi na wakuu wao wa idara. Katika kuhamishwa kwa mfanyakazi kutoka kituo kimoja kwenda kingine huwa daima sababu zifuatazo zinapelekeaga kuhamishwa kwa mfanyakazi Fulani:
1.Amehamishwa kwa kuwa ameonekana kuwa mtendaji mzuri hivyo aende akatende vivyohivyo katika eneo kingine... ambalo halina mtendaji mwingine mzuri kama huyo.
2.Ni mtendaji mbaya, ni mzembe, hivyo hilo eneo alipo hafai kufanya kazi aliyopewa, kwa maana kwamba huyo hasipohamishwa ataendelea kuharibu kazi ya serikali au kampuni, ni kwa msingi huo uhamisho wa namna hii huambatana na kubadilishiwa kazi baadala ya kuendelea na kazi hiyo hiyo.
1.Amehamishwa kwa kuwa ameonekana kuwa mtendaji mzuri hivyo aende akatende vivyohivyo katika eneo kingine... ambalo halina mtendaji mwingine mzuri kama huyo.
2.Ni mtendaji mbaya, ni mzembe, hivyo hilo eneo alipo hafai kufanya kazi aliyopewa, kwa maana kwamba huyo hasipohamishwa ataendelea kuharibu kazi ya serikali au kampuni, ni kwa msingi huo uhamisho wa namna hii huambatana na kubadilishiwa kazi baadala ya kuendelea na kazi hiyo hiyo.
3. Uhamisho ambao matokeo yake ni mgogoro/kutohelewana kati ya mwajiri/kiongozi wa idara na mwajiliwa. Daima mwajiri/kiongozi wa idara akiona kuwa mwajiriwa wake anakuwa mwerevu kumpita au hawaelewani kwa mambo Fulani kati yao, mwajili kwake hufanya kitu kidogo ili kuondoa huo mwiba ulio nyayoni mwake(mwajiriwa) Afanyacho kiongozi huyo ni kumpa uhamisho huyo mwajiliwa kwa kumpeleka maeneo ambayo huyo mwajiliwa hatoridhishwa nayo na hivyo anaweza acha hiyo kazi(akufukuzaye hakwambii toka).
Kwangu ni kwa hiyo namba tatu, kwamba kama anayehamishwa anapewa uhamisho kama adhabu, hana budi kufurahi na kushangilia maana anavyohamishwa kupelekwa mazingira magumu/hatarishi ndoo vivyo hivyo atatumia akili yake, uweza wake, na ujuzi wake kujifunza namna ya kupambana na hali ngumu. Tena faida kwa huyo ni kwamba aweza kuwa na ujuzi zaidi hata kumpita yule aliyemwamisha kituo cha kazi. Daima ukihamishwa mshukuru aliyekuhamisha hata kama ilikuwa kwa lengo baya,maana kwa jinsi hiyo anakuongezea weredi wa kufikiri na kuwa na ujuzi mpya katika kuona mazingira hatarishi kama moja ya fursa za kukusaidia kutenda vyema na kujifunza zaidi kutoka katika mazingira yaonekanayo hatarishi kwake.
Kwangu ni kwa hiyo namba tatu, kwamba kama anayehamishwa anapewa uhamisho kama adhabu, hana budi kufurahi na kushangilia maana anavyohamishwa kupelekwa mazingira magumu/hatarishi ndoo vivyo hivyo atatumia akili yake, uweza wake, na ujuzi wake kujifunza namna ya kupambana na hali ngumu. Tena faida kwa huyo ni kwamba aweza kuwa na ujuzi zaidi hata kumpita yule aliyemwamisha kituo cha kazi. Daima ukihamishwa mshukuru aliyekuhamisha hata kama ilikuwa kwa lengo baya,maana kwa jinsi hiyo anakuongezea weredi wa kufikiri na kuwa na ujuzi mpya katika kuona mazingira hatarishi kama moja ya fursa za kukusaidia kutenda vyema na kujifunza zaidi kutoka katika mazingira yaonekanayo hatarishi kwake.