Jumanne, 20 Oktoba 2015

MAADILI JUU YA AHADI.

Ahadi yaweza kuleta matumaini ya kuishi kwa muda mrefu bila ya kuona ukweli wenyewe au uhalisia wa hiyo ahadi.Kwa kifupi naweza sema ahadi siyo tofauti na ndoto maana hivyo vyote ni ishara zinazolenga kwenye uhalisia japo zenyewe siyo uhalisia(reality)kamwe. Ahadi ni kama vile mtu kusikia harufu ya chakula kikipikwa au kukaangwa akasikia kushiba kumbe ihali bado ana njaa ya kutosha. Sasa wengi wetu ndo hali tuliyoifikia wakati tukielekea uchaguzi mkuu.Hivi hizi ahadi zinazotolewa na waheshimiwa tukapiga makofi kwa nguvu tukafanana na waliokwisha kula na kushiba, hivi huu ni ukweli na uhalisia au bado tuko kwenye ndoto?.Kuna namna nyingi zakudanganywa na ukakubali kiulaini bila ya manunguniko.Njia mojawapo ni ahadi ambazo ni nusu ya uhalisia na nusu uongo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni