Jumanne, 20 Oktoba 2015

KWA NINI WALIMU WANAPATA UJIRA WA KUBABAISHA?

Tujiulize swali la msingi kuwa kama walimu wetu wangelikuwa wanalipwa posho kama za wabunge kwa mwezi kungelitokea nini katika sekta ya elimu?Hivi huyu anayeenda kuwakilisha wananchi katika chombo cha dola ambacho ni moja ya mihili mikuu ya serikali kimaarifa au kielimu huyu inasemwa kuwa walau awe na elimu ya kidato cha nne na zaidi ajue kusoma na kuandika basi. Cha kushangaza na kuchekesha ni kuwa huyu ambaye anasemwa kuwa ajue kusoma na kuandika mara nyingi huwa tunawaona kupitia Luninga wakiwa wamechapa usingizi na kusahau kile kilichowafanya wawe hapo;kisa ni kujua kusoma na kuandika na mwishowe huyo anapata posho Mara nne au tano ya mwalimu au mtu yeyote mtaaluma ambaye kila siku lazima asumbue kichwa chake kufanya kazi Fulani,wakati waheshimiwa wanalala na posho inaingia.Hivi ninani ambaye hawezi simama pale bungeni na kutoa hoja? kusimama pale kunahitaji kuumiza vichwa kweli?jibu ni hapana ila kukaa pale ni sawa na kusema kama waswahili wa mtaani wasemavyo"kula kuku kwa mrija." Hii itakuwa sahihi nikisema kuwa baadhi ya wataaluma wetu hasa maprofessa wetu wa vyuo vikuu wanaacha fani zao na kukimbilia kwenye siasa maana huko kuna ulaji kwa njia ya mtelemko bila ya kusumbua vichwa.Hivi kama hao wanaokimbia fani zao na kuingia katika siasa wangelikuwa wanapewa keki wanayopewa hawa waheshimiwa bungeni tungelikuwa hatua ya juu sana kielimu. Uwezo wa kujenga hoja na fikra hautegemei kusoma na kuandika,Bali unahitaji pia nguvu ya kufikiria na kujenga hoja makini.Wale waliopaswa kushauri wanaoongoza pia nao wanataka kuongoza,je hapo nani atatoa maoni na ushauri kwa wanaoongoza?matokeo yake ni kuishia katika ushabiki usiojenga

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni