Jumanne, 20 Oktoba 2015

KWA NINI KUTAWALIWA NA HISIA BAADALA YA KUTAWALIWA NA UFAHAMU?

Ni jambo la kushangaza kuona watu wanatawaliwa na hisia(feelings) za wengine na kuzifanya hisia zao.Kimsingi kundi la watu wa namna hiyo linakuwa limepoteza malengo na mwelekeo kwa ujumla katika maisha.Ukiangalia ushabiki unaofanywa kwa sasa katika vyama vya siasa unaweza tambua kuwa sio mashabiki wote wanajua walitendalo ila wengi wao huenda kwa mkumbo wa kwa kuwa Fulani kashabikia hebu na Mimi nishabikie kitu ambacho ni hatari katika maendeleo na utu wa kila mmoja wetu.Hivyo hatuko mbali kusema kuwa ushabiki ninamna ya watu kuishi maisha ya wengine ili mradi siku ipite.Ushabiki lazima uwe na tija na malengo pia ya kumnufaisha mwananchi kuliko kumnufaisha mgombea.Ni heri kutoshabikia yale tusiyoyajua maana wanaofaidika ni wengine.Kwa jina la ushabiki wengine wameshanunuliwa kwa kilauri/kiloba wakiwa wamesahau kuwa wanauza utu wao na haki zao kwa vitu vya mpito visivyokumbukwa daima.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni