Jumanne, 20 Oktoba 2015

ELIMU NA UMUHIMU WAKE

Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni