Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu
mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana
na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa
uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika
mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji
waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke
kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi
mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya
kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi
weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa
nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia
ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao
walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai
wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert
na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na
kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia
zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora
za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu
wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao
hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi
wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa
mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila
mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi
akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana
ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni