Inashangaza kuona watu wanambiwa na kupewa ahadi kuwa wataondolewa
umaskini na kuwafanya wawe na maisha mazuri. Umaskini wanaouongelea
waheshimiwa ni umaskini upi?kuna umaskini wa fikra, umaskini wa njaa,
umaskini wa hela, na umaskini wa elimu,sasa waheshimiwa wakisimama
kuwapigia watu tarumbeta ya kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini mbona
hawaelezei namna na jinsi watakavyo mfanya kila mtanzania aondokane na
umaskini wa aina zote zilizotajwa hapo juu?inawezekana ukawafanya
watu wote nchi hii wakawa kweli matajiri au ni siasa inayosukuma hayo
mambo kuliko utawala wa akili na kufikiri juu ya hao waheshimiwa
wayasemayo?Hata nchi zilizoendelea bado zina maskini,inakuwaje sisi Leo
tuambiwe kuwa baada ya uchaguzi tunakuwa matajiri bila hata ya
kuonyeshwa ishara halisi kimatendo ila kwa maneno ndo kwingi?Hayo yote
ni kuongelea mdomoni kuliko kongelea akilini.
Jumanne, 20 Oktoba 2015
UMRI WA UZEE NA MAHITAJI YAKE
Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee
anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo
asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba
au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na
hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na
wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu
kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama
msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa
mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe
pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi
wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto
ELIMU NA UMUHIMU WAKE
Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu
mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana
na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa
uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika
mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji
waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke
kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi
mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya
kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi
weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa
nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia
ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao
walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai
wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert
na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na
kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia
zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora
za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu
wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao
hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila
mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi
wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa
mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila
mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi
akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana
ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao
JIBADILISHE KABLA HUJABADIRISHWA
Itawezekana kupata mabadiliko ikiwa wanaodai hayo mabadiliko hata wao
wenyewe hawajajiletea mabadiliko hata kwa mambo madogo waliyonayo?mfano
kama mtu anadai mabadiliko wakati hata magugu yaliyozunguka nyumba yake
yanamshinda kuyangoa, mtu akishindwa kufagia nyumba yake na kuipanga
vizuri na hata akashindwa kupanga chumba chake anapolala mwenyewe sasa
ukisikia huyo anadai mabadiliko huyo kweli anadai mabadiliko kutoka
ndani ya moyo wake au ni msukumo wa mikumbo ili mradi siku
imeenda?Itawezekana kweli kudai mabadiliko ihali mdai mabadiliko
hajajibadilisha na kubadilika na hatimaye kudai ili abadilishwe
zaidi.Kamwe haitowezekana mabadiliko kwa watu kama watu wenyewe
hawajajibadilisha katika vitu vifuatavyo:1.Kujibadilisha kifkra
2.Kujibadilisha kimtizamo hasa juu ya kufikiri,kutenda, na kuchukulia
uhalisia wa mambo.3.Kujenga mtizamo chanya na kujikubali mapungufu
4.Kuondoa dhana ya kujihisi wanyonge daima na hivyo kujenga dhana ya
kuwa wategemezi daima. Kwa hili ni kuwa dhana ya kutegemea kila kitu
kupewa ndo wengi tumejikuta tunaitwa mbumbumbu na hivyo kutengeneza
mwanya kwa waheshimiwa kutoa ahadi hewa za mabadiliko
yasiyokuwepo.Tusipojibadili namna ya kuchukulia na kufanya mambo
tutajikuta hatuna mabadiliko kamwe.Haiwezekani ukalala bila ya kufanya
lolote na hapo ukategemea mabadiliko yatokee.Kuleta mabadiliko ni moja
ya mapinduzi katika historia.Tukumbuke kuwa hustoria ni kwa wale tu
waitengenezayo(history is only for those who make it,never sleep and
expect history to be made for you).Mabadiliko yatakuja pale ambapo
tulisha anza sisi wenyewe kwa Yale madogo tuliyoanzisha kwa juhudi zetu
wenyewe
LUGHA NA MATUMIZI YAKE
Matumizi ya lugha isivyo hitajika yaweza kupoteza ukweli wa mambo
kihalisia na kufanya hata watu wasiohusika hata vitu visivyoweza kutumia
ufahamu(reasoning) kuonekana kuwa vina hatia. Mara nyingi tumeshuhudia
mfano ajali nyingi hapa kwetu na duniani kote.Ajali kama hizo
zimehusisha watu kupoteza maisha kutokana na hizo ajali. Mfano
tumeshuhudia ajali za vyombo vya moto kama vile pikipiki na magari,
ndege,na vinginevyo. Jambo ambalo huwa daima linanishangazaga ni kwenye
mawasiliano wakati wa kutoa taarifa
baada ya kutokea ajali mfano utasikia mtu anaongea kuwa " nimeangushwa
na pikipiki,au nimeangushwa na gari" hivi kweli hii inawezekana
kimaongezi kuwa mtu ameangushwa na pikipiki au gari? mimi naona kuwa
hiyo siyo sahihi kamwe.Daima mtu huwa ndo anaiangusha pikipiki au gari
maana hivi vifaa vya usafiri huwa havina akili au utashi wa kuamua
kumdondosha mtu bali uzembe wa mtu huwa ndo unamfanya adondoshwe au
aangushwe na hicho kifaa cha usafiri.Hiyo ndo kawaida yetu binadamu kuwa
huwa hatupendi kuwajibika kutokana na uzembe wetu baadala yake ni
kuhamishia maumivu na hisia kwa watu na hata vitu visivyo na uhai
kuhusika na mikosi tuipatayo. Nimesikia mara nyingi mtu mmoja akisema
kuwa kamwe hatopanda pikipiki, nilipomuuliza sababu ya kusema vile
akaniambia kuwa ni kwa kuwa pikipiki zimeangusha na kuua watu
wengi;swali langu kwake lilibaki kuwa " je pikipiki huwa inaangusha mtu
au mtu huwa ndo anaiangusha?" Uwajibikaji ni muhimu kabla ya kuelekeza
tuhuma kwa wengine.
KWA NINI WALIMU WANAPATA UJIRA WA KUBABAISHA?
Tujiulize swali la msingi kuwa kama walimu wetu wangelikuwa wanalipwa
posho kama za wabunge kwa mwezi kungelitokea nini katika sekta ya
elimu?Hivi huyu anayeenda kuwakilisha wananchi katika chombo cha dola
ambacho ni moja ya mihili mikuu ya serikali kimaarifa au kielimu huyu
inasemwa kuwa walau awe na elimu ya kidato cha nne na zaidi ajue kusoma
na kuandika basi. Cha kushangaza na kuchekesha ni kuwa huyu ambaye
anasemwa kuwa ajue kusoma na kuandika mara nyingi huwa tunawaona kupitia
Luninga wakiwa wamechapa usingizi na kusahau kile kilichowafanya wawe
hapo;kisa ni kujua kusoma na kuandika na mwishowe huyo anapata posho
Mara nne au tano ya mwalimu au mtu yeyote mtaaluma ambaye kila siku
lazima asumbue kichwa chake kufanya kazi Fulani,wakati waheshimiwa
wanalala na posho inaingia.Hivi ninani ambaye hawezi simama pale bungeni
na kutoa hoja? kusimama pale kunahitaji kuumiza vichwa kweli?jibu ni
hapana ila kukaa pale ni sawa na kusema kama waswahili wa mtaani
wasemavyo"kula kuku kwa mrija." Hii itakuwa sahihi nikisema kuwa baadhi
ya wataaluma wetu hasa maprofessa wetu wa vyuo vikuu wanaacha fani zao
na kukimbilia kwenye siasa maana huko kuna ulaji kwa njia ya mtelemko
bila ya kusumbua vichwa.Hivi kama hao wanaokimbia fani zao na kuingia
katika siasa wangelikuwa wanapewa keki wanayopewa hawa waheshimiwa
bungeni tungelikuwa hatua ya juu sana kielimu. Uwezo wa kujenga hoja na
fikra hautegemei kusoma na kuandika,Bali unahitaji pia nguvu ya
kufikiria na kujenga hoja makini.Wale waliopaswa kushauri wanaoongoza
pia nao wanataka kuongoza,je hapo nani atatoa maoni na ushauri kwa
wanaoongoza?matokeo yake ni kuishia katika ushabiki usiojenga
MAADILI JUU YA AHADI.
Ahadi yaweza kuleta matumaini ya kuishi kwa muda mrefu bila ya kuona
ukweli wenyewe au uhalisia wa hiyo ahadi.Kwa kifupi naweza sema ahadi
siyo tofauti na ndoto maana hivyo vyote ni ishara zinazolenga kwenye
uhalisia japo zenyewe siyo uhalisia(reality)kamwe. Ahadi ni kama vile
mtu kusikia harufu ya chakula kikipikwa au kukaangwa akasikia kushiba
kumbe ihali bado ana njaa ya kutosha. Sasa wengi wetu ndo hali
tuliyoifikia wakati tukielekea uchaguzi mkuu.Hivi hizi ahadi
zinazotolewa na waheshimiwa tukapiga makofi kwa nguvu tukafanana na
waliokwisha kula na kushiba, hivi huu ni ukweli na uhalisia au bado tuko
kwenye ndoto?.Kuna namna nyingi zakudanganywa na ukakubali kiulaini
bila ya manunguniko.Njia mojawapo ni ahadi ambazo ni nusu ya uhalisia na
nusu uongo.
KWA NINI KUTAWALIWA NA HISIA BAADALA YA KUTAWALIWA NA UFAHAMU?
Ni jambo la kushangaza kuona watu wanatawaliwa na hisia(feelings) za
wengine na kuzifanya hisia zao.Kimsingi kundi la watu wa namna hiyo
linakuwa limepoteza malengo na mwelekeo kwa ujumla katika
maisha.Ukiangalia ushabiki unaofanywa kwa sasa katika vyama vya siasa
unaweza tambua kuwa sio mashabiki wote wanajua walitendalo ila wengi wao
huenda kwa mkumbo wa kwa kuwa Fulani kashabikia hebu na Mimi nishabikie
kitu ambacho ni hatari katika maendeleo na utu wa kila mmoja wetu.Hivyo
hatuko mbali kusema kuwa ushabiki ninamna ya watu kuishi maisha ya
wengine ili mradi siku ipite.Ushabiki lazima uwe na tija na malengo pia
ya kumnufaisha mwananchi kuliko kumnufaisha mgombea.Ni heri kutoshabikia
yale tusiyoyajua maana wanaofaidika ni wengine.Kwa jina la ushabiki
wengine wameshanunuliwa kwa kilauri/kiloba wakiwa wamesahau kuwa wanauza
utu wao na haki zao kwa vitu vya mpito visivyokumbukwa daima.
NANI AHUDUMIWE NA NANI ALALAMIKIWE?
Kama wanaohudumiwa wanawalaumu na kuwalalamikia sana wanaowahudumia, je
wanaohudumia watahudumiwa na nani?na wakilalamikiwa nawao watamlalamikia
nani? Siyo vema kulaumu na kulalamika kilawakati maana na hao
wanaolalamikiwa wana haki ya kulalamika nao ni binadamu kama binadamu
wengine.
MIFUMO NA MADHARA YAKE
Kuna wengi ambao kiutendaji huonekana wema.Tatizo linakuja pale ambapo
utendaji wao unazoroteshwa na kumezwa na mfumo mama uliowalea hadi
wakaota vitambi na mvi.Hao watendaji daima huishia kuumia na kuzikana
nafsi zao ili waendelee kulea na kubeza mifumo iliyowalea hata kama
wanaona kuna mapungufu.Wakijaribu kuinua na kupaza sauti zao wanajikuta
wanalaumiwa na kulumbambana na hao wazazi wao(mifumo)iliyowalea.Mifumo
ipo na inaendelea kuwepo katika jamii ili iendelee kuneemeka.Waendao
tofauti na mifumo hao ndo wanaonekana kukimbilia upande mwingine wa
shilingi. Pia ikumbukwe kuwa mifumo imetawala nyanja mbalimbali mbali
katika jamii yetu. Wale ambao wanaonekana wema na watakatifu na
wanaopaza sauti zao wakilalamikia mifumo iliyopo kwa sasa, wakishapewa
nyenzo tutashuhudia mda si mrefu wao watajenga mifumo ya namna
gani?either mfumo wa kujifaidisha wenyewe au mfumo kwa ajili ya manufaa
ya wote?lazima tutambue kuwa binadamu ni fumbo ambalo halijafumbuliwa na
lisilo rahisi kueleweka kwa kila mtu.Yule anayelia na kuwafanya wengine
walie,je wale waliao wakimfikisha mliaji anapotaka je wao wakianza
kulia atawasindikiza na kuwafikisha wanapotaka(wananchi)?Wanaoonekana
kuomboleza wakisha fikishwa mahala pao wanapotaka daima hujenga kuta ili
kuwazuia waombolezaji wasiingie pale walipofika(Ikulu).Tusikumbwe daima
na mikumbo ya kutekwa na kuwa watumwa wa mifumo tusiyo ijua malengo
yake.
UCHAGUZI MKUU UMETUFIKIRISHA NINI?
Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo
kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo
kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao
waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga
ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi
watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu
mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani
alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama
chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika
chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au
watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa
wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake,
kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni
mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona
wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo
kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa
watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama
ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi
waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita
kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha
kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika
kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa
kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of
generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na
baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.
MCHEZO WA SIASA NI MCHEZO WA NAMNA GANI?
Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo
kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo
kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao
waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga
ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi
watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu
mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani
alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama
chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika
chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au
watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa
wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake,
kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni
mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona
wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo
kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa
watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama
ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi
waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita
kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha
kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika
kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa
kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of
generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na
baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.
HUU NI WENDAWAZIMU KUPIGA BARABARA DEKI AU?
Nijambo la kutafakarisha kuona watu wanapiga barabara deki tena kwa
nguvu zote! na hili kimsingi siyo jambo la kawaida hata kidogo.Waweza
jiuliza nini kinawasukuma watu kufanya hivyo?je wanafanya hivyo kwa
ushabiki au kufanya hivyo kunaashiria jambo Fulani? Kama tujuavyo watu
wakifanya hivyo wanakuwa wanaashiria jambo fulani kwa kutarajia litokee
na kuwafanya wawe katika hali fulani ya maisha. Tunajua kabisa kuwa
alama zionyeshapo uendapo huwa daima zinasaidia kuonyesha mahali
sahihi unapohitaji kwenda japo alama zenyewe siyo mahali unapotaka
kwenda. Tukiona watu wanapiga deki na kupangusa Barabara wanakuwa hasa
wanatoa ishara gani? hapo twaweza kuwa na majibu na fikra nyingi.
Mojawapo ikiwa ni kwamba wamechoshwa na mfumo mbovu wa uongozi wanataka
uongozi mpya na dira mpya ya maendeleo, au kwamba wananchi wanataka sasa
kupumulia mahala pazuri pasipo hila wala uyanganyi wala ufisadi n.k
hayo ni baadhi ya majibu waliyonayo wapiga kura.Kiuhalisia siyo jambo la
kufikirika watu kutumia mda wao mwingi kusafisha barabara pasipo
kuambiwa kufanya hivyo au pasipo malipo isipokuwa kuna jambo fulani
ambalo kwa wasio funguka macho bado ni kitendawili.
MTU NA UTU WAKE
Ukitaka kutambua utu wa mtu na kumjua yeye ninani mpe Uhuru wa umfanyie
nini?hapo ni dhahiri kuwa utapata majibu mengi kutoka kwa huyo mtu juu
ya analotaka umfanyie hata kama mengine yapo juu ya uwezo wake.Katika
nafasi hiyo utapata kutambua kama huyo mtu ni mchoyo na pia mwenye uchu
wa kutaka kutawala au pia utapata kujua unyenyekevu wa huyo mtu kadiri
ya kitu ambacho amekuomba ukamfanyie.Sasa tuje ngambo nyingine ya
Shilingi ambapo Leo hii tumeshuhudia wale waliokuja kutuomba
dhamana ya kuongoza nchi.Wao wakati wanahangaika ili tuwape dhamana ya
kutuongoza mambo yamekuwa kama ifuatavyo:1.Wao wamekuja na bado wanazidi
kuja kwetu na tumewauliza "je mwataka tuwafanyie nini?" Wao wakajibu
kwa sauti kubwa "mtupigie kura ya ndiyo katika uchaguzi mkuu
ujao."2.Pindi na sisi ilipokuwa zamu yetu juu ya wao watufanyie nini,
wamekuja na majibu mbalimbali yenye kutia moyo japo hayana uhakika
asilimia mia moja.Moja ya majibu mepesimepesi ni kufuta baadhi ya Kodi,
Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.Kuanzisha viwanda,
kuhakikisha kuwa vijana wote(waliosoma na wasiosoma)wanapata ajira na
wanakuwa na maisha mazuri n.k.Hayo yote ni mazuri sana ila wengi wetu
tunasahau kuwa siyo kila ahadi utekelezeka! Kwa Mawazo yangu ni kuwa
itakuwa rahisi kwetu kutoa majibu ya maswali yetu ya tuwafanyie nini
waheshimiwa maana majibu yanaeleweka, kuwa tutawapigia kura ya
ndiyo.Wasiwasi unakuja kwa majibu ya maswali yetu kwao kuwa watatufanyia
nini?majibu yao kwetu yamekuja na ahadi ambazo ni vigumu kuamini kuwa
zitatekelezeka.Tunasahau kuwa Siasa ni mchezo ambao siyo wote twaweza
kuucheza. Punde tutashuhudia kama tulidanganywa juu ya hizo ahadi au la!
wakishapewa hayo majukumu ndoo itakuwa kutekeleza au kutokuteleza hizo
ahadi.Hofu yangu ni kwamba kwa nchi kama Tanzania,Ahadi zilizotolewa
baadhi ziko nje ya uwezo wake, kama vile Elimu bure na ajira kwa kila
mtanzania hasa vijana.Hayo yote ni majibu ya tutafanyiwa nini.Yatubidi
tufunguke macho na kuelewa kati ya kuambiwa ukweli au kulaghaiwa.
LUGHA YA BAO LA MKONO
Kwa sasa tunaambiwa lugha ya bao la mkono! bao la mkono halikulezewa
vizuri na kuzungumzika vizuri.Mtoa hoja angelielezea vizuri ni mchezo
gani ambapo bao la mkono ni marufuku mfano katika kucheza mpira wa miguu
ukifunga bao la mkono jua kuwa kuna adhabu juu yake(Penalty) wakati
kama unacheza Mpira wa mikono(volleyball au Basketball) gori la mkono
hapo hapo halina shida. Shida ni pale bao la mkono linafungwa wakati wa
mchezo wa mpira wa kutumia miguu.Afungaye kutumia mkono kwa
mchezo wa Mpira wa miguu hapo inamhitaji abadilike. Katika mfumo wetu
wa utawala yaonekana wananchi wameumizwa vibaya na kufikiria vinginevyo
kwamba mabao yanayofungwa siyo halali kwa kuwa mchezo unaochezwa ni
mchezo wa mpira wa miguu lakini bado mabao yanayofungwa ni ya mkono
pasipo halali(utumiaji wa nguvu kupita kiasi na rushwa).Bao la mkono
litatambulika kuwa hivyo na halali pindi mchezo ukiwa wa kuchezwa kwa
mikono na siyo miguu.Kama wananchi wanalalamikia bao la mkono hii
inamaana gani? kwamba mchezo unaochezwa ni wa miguu ambao kiutaratibu
lazima bao kama bao linafungwa kwa miguu,Ila matokeo yake washangiliaji
wanaona bao linafungwa kwa mkono wanashangaa na kufikiri kutowezekana
kwa hilo bao lililofungwa na wakati huo refaree anaweka tiki kuwa ni bao
stahiki mbali ya kujuakuwa siyo halali.Tujiulize kuwa katika uwanja wa
Siasa wachezaji wanacheza mchezo gani? wa kukubali mshindi halali au
lile bao la mkono?
Ijumaa, 29 Mei 2015
WHY TO RISK FOR NO APPARENT REASON?
"Never be separated and torn apart by people's differences whose source is not your concern"
Ijumaa, 22 Mei 2015
THE FALL OF A BIG MAN
"The fall of honourable person in the society is always accompanied by a big bang"
FR. REVOCATUS PAUL'S QUOTATIONS
“In a moment when truth is being derivered to those who have been
deprived of it, on their part it becomes a joyous moment but on the contrary
when the same truth is delivered to the counterpart it becomes a bitter
moment,Yet the same truth once not accepted it makes a step a head of the one
who has rejected to embrace it. Accepting a truth is not instantenous process,
it is a gradual process.In one way or another no body here on Earth has dared
to embrace the absolute truth.What majority embrace is that which seem to be
equivalent to truth.However truth with time should be embraced either in calm
moments/displeasurablemoments.Those who have mismanaged truth I dare to call
them liers.”
“Money is a decorated house for the devil.The devil welcomes those who
abuse the use of that commodity called money into his decorated house.Thus
money is the hidden trapof a devil waiting to catch those who mismanage it.”
“You can't climb the ladder of achievement
while hands are on your pockets” (C.Niger)
“Lawless society/community will result into
powerless against powerful individuals.The voice of the voiceless will never
penetrate the voice of powerful individuals in a lawless society.Those in power
are becoming ambitious to alter the constitutions of their respective countries
to ensure that they remain in power for ever.Such people tend to think that
they were born alpha and omega presidents.In Africa majority of our countries
are ruled under the umbrella of democracy while in real sense what is happening at the ground is a drama of
surviving for fittest vs weak people. What's really at stake in African
politics is the gymnastic competition of those having strong teeth to tear
aflesh against toothless individuals, honestly speaking who will win the
competition?definitely are the ones having strong teeth to tear flesh on their
predators(citizens).Our Leaders unlawful become presidents under Machiavel's
principles(The end does not justify the means-If you want to be a leader make
sure that you become,e.g if it's through shedding blood of Innocent people that
is not a problem what matters is for an individual to become a leader).Let's
pray for our dear brothers and sisters who are tormented by such system of Political
ruling system without excluding Burundi,Zimbabwe,Uganda to mention but few.”
“Giving out of charity is moral and religious
obligation on the part of the donor,but on the part of the recipient is not
obligation, the constant charity donation to the recipient on the other hand
turns out to be mandatory on the part of the donor.The recipient because of
constant receiving charity from the donor turns it out to be obligation even if
the donor has nothing to give yet the recipient will keep on demanding to be
given even what is not there. When a recipient has not tested how to have what
is given is found he/she won't stop demanding much.In order to let the
recipient who has been given charity freely test how it is found never give
him/her fish, rather teach him/her how to fish.”
“It's good to hear people's advices,yet it is
dangerous to be at people's disposal,once you accept that condition of being at
one's disposal it means you are owned as any other property,you are no longer
free to express the freedom of your conscience. Being at peoples disposal is
slavery created unknowingly/knowingly. Because of poverty majority have found
themselves victims of being owned like any other property while in real sense
they are both conscience and thinking beings(rational animals)”
“It is surprising that we have what we call
university Lecturers,Doctors,and Professors, some of these academicians have
been given these academic titles undeservedly.If you have done
tertiary(university education) It's my hope that you have realized that some of
the mentioned people above hold academic credentials they are not supposed to
hold. The cause of this is due to fact that in their teaching and presenting
materials to their students they seem to be not what they hold as their academic status. Poor presentation of staff to
the students is an indication that a Professor/Lecturer/Doctor was not
qualified to that title because of the following reasons:1.In the course of his
study he/studied the course by claiming and memorizing without understanding
the core subject at hand. 2.Plagiarism:In this fact majority falls to this
category,this concerns those who copy other peoples works and acknowledge them
as their original work.Some even have dared to copy and paste peoples thesis
and dissertations and thus acknowledge them as their original work for academic
credit.This is what we call an intellectual theft! down the centuries these
people have been there and are still there eating where they have not sown.This
to say is not different from other graft public scandals.Academic
irregularities and dishonest is a big scandal beyond corruption scandal.Our
government is silent on such people being in our universities and public
offices holding the titles they do not in fact deserve. The government should
be courageous to take the disciplinary measures against these people.Yet the
challenge ahead is that who will fix the bell at cat's neck??those holding high
public offices are the one in front line being victims of academic
irregularities and dishonest! who is able to confront the other? Corruption has
become an incurable disease that is eating our institutions?will PCCB be able
to deal with these intellectual robbers in our universities and public offices?”
“Wahubiri siyo kazi yenu kuhubiria waumini wenu
na kisha kuwaacha mawinguni Bali wahubirieni hadi mkawafikishe
mbinguni(Polepole kwenye semina ya kura ya maoni ya Katiba pendekezwa jumbo kuu
Katoliki la Arusha)”
"A good speach is motivated by prior
preparation of an occassion to be discussed."
“It's useless and silly to be critical on other
affairs that won't benefit you at all.Critical minds are the one's that seek to
construct and not to destroy what has been already constructed. If you can't
construct never attempt to destroy ready made reality /thought”
“The use of mobile phones has facilitated many
things to be done in a short period of time.This has made communication to be
easy as we can imagine.The use of this technology has somehow to a greater
extent replaced the local method of communication like postage communication,
and Landline telephone communication system.All in all we have the courage to
thank God for having enlightened the scientists mind to discover such an easy
communication facility.However,there has been shortcomings due to use of this communication technology,to
mention few examples,it has been found that the use of mobile technology in
facilitating communication also has resulted into cyber crimes like theft, the
use of this technology has also resulted into illegal marital affairs (breaking
of marriage),it has resulted also into psychological in equilibrium due to
mismanagement of the communication facilities.There are many things that have
to be discussed concerning the abuse use of the communication facilities.”
“When being invited by your relative/friend to
an ocassion never refuse to attend that event, the event may once change your
way of thinking and your way of looking at things. Availing at an occasion does
not necessarily mean to eat and drink,but it also mean meeting people and
exchange World's view and life reality.through this process,thus when you
attend an occasion it is also a chance for personal transformation and maturity.”
“Kwenye jamii hawakosekanagi watu wa kulaumu wengine hata wakikosa wa
kulaumu basi wao hulaumu kuwa kwa nini waliumbwa? Watu kama hao ndo waitwao
wale watafutao ukamilifu na mambo yote kwao huwa wanataka yawe
makamilifu(Perfectionist people) hawa huwa hawakubali mapungufu ya wenzao ila
huwa wanapenda ukamilifu kwa wengine.Hivyo kundi hili la watu wapendao kuona
ukamilifu(perfection in others) wanakuwa siyo rahisi kuishi na kuelewana na
jamaa na rafiki zao.Ni kwa msingi huu tunaona kuwa watu wa
namna hii siyo rahisi kuwa na marafiki wengi kwa kuwa wao huona kila mtu siyo
mkamilifu kama wao watakavyo.lawama na kuwalaumu wengine kuwa wamekosea bila
hata kuangalia mazuri yao huwa kwa wakati mwingine inamfanya huyu apendaye
ukamilifu kwake na kwa wengine daima aishi ulimwengu wake aujuaye yeye. Na kwa
kutengeneza ulimwengu aujuaye huyo atakaye ukamilifu si ajabu wale wasio
wakamilifu oia nayeye wakaona mapungufu yake na hivyo kupelekea kuitwa mwenye
akili sana au mwendawazimu. Heshima kwa utu wa mtu yakiwemo mazuri na mapungufu
ya mtu huwa ndo vinajenga utu wa mtu.Vile avifanyavyo mwanadamu huwa ndo
vinajenga na kubomoa utu wake.Utu wa mtu kwa ujumla ukamilishwa na mahitaji
yake ,mazingira,na oia watu aishio nao. Mtu asiposifiwa kwa yale ayafanyayo utu
wake unakuwa umefananishwa na yule mtu aonaye dhahabu iliyochanganyikana na
matope akaamua kuitupilia jalalani baadala ya kuondoa tope ns kuchukua dhahabu.
Vivyo hivyo mtu akiwa na mapungufu siyo kuwa ni mbaya,upande mwingune wa
Shilingi ni kuwa mtu huyo mabaya yake yakiondolewa bado anamazuri ya kunufaisha
jamii.Hivi ni wangapi wametupwa majalalani na mazuri yao wakidhaniwa kuwa ni
wabaya wakutupwa???Tutafakari juu ya hilo.”
“Ukikutana na yule usiyemjua njiani
usimcheke/kumdharau/kumsengenya kwa namna alivyo kwa kuwa huyu aweza akawa
anaenda nyumbani kwako na pia aweza kuwa mtu mashuhuri ambaye siku zote umekuwa
ukisikia habari zake na pia ungelipenda kukutana naye siku moja.Kumbuka kuwa
cheo cha mtu huwa hakimbadilishi sura,ila watu wamjuaye huyo mtu huwa ndo
wanampaka sura kutokana na cheo chake na matendo yake kwenye jamii aishiyo.”
“Don't look at rich people and think that they
became rich within a day, their state of being rich has left the history
behind! If you attempt to examine, and analyse their history of how they got
there, somehow the nature by itself will tell you a lot concerning Histories of
such rich men, which include good and bad histories.All in all History remains
a history despite of its good/bad attributes.History is for those who make it.”
“If you want to know who is a real friend to
you, just mention your problem to him/her.From his/reaction it's when you will
notice his/her concern to you.”
“Binadamu daima huwa hakosi kisingizio.Akikosa
kumsngizia mwanadamu mwenzake basi atasingizia utupu,giza na mwanga.”
“A man who said to have been a university
graduant was some where looking for an employment, thanks be to God in his
going around he saw an advatisement inviting candidates of his qualifications
to appy for a job on that particular company, a man being delighted went with
his credentials ready for an interview, reaching at the gate of the company he
found a very simple and short Man standing at the gate talking to a Watchman,
when a man being asked what was he looking at the Company a man unhestatingly replied" I want to meet a boss of this
Company, I am having an issue with him" the simple and short Man at the
gate asked him " which issue are you having with him?" A man replied,
" sorry it does not concern you, please tell me if the boss is around or
he is not around? and don't waste my time". As the interogation was going
on between the university graduant looking for a job in the company, and the
short Man, thus a confrotation between the two arose. At the end of long
argument and confrotation, the short and simple man revealed himself that he
was the company's boss. He told a university graduant that he had already
failed an interview! Lesson. Pay respect to people you meet because you never
know that when you are looking for something they are the ones to find that
thing for you. Being wise and prudent in dealing with others is passmark for
our daily interviews.”
“Everybody who is idle, potentially is the
green pasture where the devil may be fed on.”
“When people don't speak something about you,
don't think that they don't know you, your way of life(Moral conducts) will
reveal to people who are you, this qualifies people either to talk good things
about you or to talk evil things about you. Nevertheless, the challenge here is
that majority prefer to speak scandalous news about others instead of good
news! what pushes them to act like that? It's because the devil has been at
work and is at work to ensure that good minds are corrupted in a way that they
can't see goodness on others.”
“The way you are( Physical make up,
Psychological make up, mental make up, social make up) is the way God wants to
communicate to others and make them learn from you. Don't disapprove God for
having created you the way you are, He has got purpose to create you,the plan
of God to our life is beyond our intellectual grasp. Let God fulfill His plans
and Purposes in our life. Remember that Comparison in life breeds contempt. God
has created every body in a unique way in order to accomplish the design of His
creation.”
“Human beings are only beings but are beings
after the attention and understanding of meaning in life.”
“Evil men should not be blamed for corruting
the World,rather those who have to be blamed are those people keeping quite
amidist of evil men without any discplinary action thus creating an evironment
for evil doers to flourish.”
“Society without regulations& laws is like
life in a zoo.”
“Food for thought: Just think ten years ago had
you ever thought to be where you are and do what you are doing now? have you
ever thought what will you be doing at the time like now for the next ten years
to come? if the answer is Yes,then how do you know it? If the answer is no,then
submit your hopes&expectations into the hands of God.”
“The truth said by our elders to avoid a
certain ways of conduct can't be accepted instantly. The truth foreseen by our
elders never fade away, it rather proceeds a head, extra mile. It awaits to
reveal by itself when the circumstance foretold by the elders to be avoided
reoccurs. The truth is ever a head of Man's thinking. Let a truth be a truth. A
lie will never complement a truth.”
“What makes people to love or to hate one
another is not one's physical make up, rather it's one's bodly languages and
ways of conduct. By nature man is born good, nevertheless,after being brought
fourth in a society, thus he/she becomes corrupted by societal influences.”
“In order to know man's humbleness and
responsibleness , two prerequisites are need .1. Let him/her be left free to do
whatever he/she likes 2. Let him/her be given a mandate to exercise his/her
freedom on others.”
“Two brick's makers were found making bricks
when were asked what were they doing one replied"I am building a
cathedral, the other replied "I am mixing sand and cement to make bricks,
between the two who gave a correct answer?”
“Kuna bwana mmoja ambaye ukimwangalia kutoka
kwa mbali alikuwa anapendeza
sana, ila ukimkaribia kidogo sura yake na maumbile kidogo vilikuwa vya kutatanisha. Kope za macho yake ni kama za mbuzi, ndevu kama mashurubu ya paka, mwili wake mzima ulijaa manyoya na vitu vingine vingi. FUNDISHO. Ukitaka kumjua mtu ninini na ninani usiishie kumtazama kwa mara moja ila kaa naye na uishi naye hapo utaona mengi na kujua mengi kutoka kwake bila ya kuacha mashurubu ya
paka nyuma.”
sana, ila ukimkaribia kidogo sura yake na maumbile kidogo vilikuwa vya kutatanisha. Kope za macho yake ni kama za mbuzi, ndevu kama mashurubu ya paka, mwili wake mzima ulijaa manyoya na vitu vingine vingi. FUNDISHO. Ukitaka kumjua mtu ninini na ninani usiishie kumtazama kwa mara moja ila kaa naye na uishi naye hapo utaona mengi na kujua mengi kutoka kwake bila ya kuacha mashurubu ya
paka nyuma.”
“Naturally we are all born free,and uncorrupt.
We are all sons and daughters of the same Father,
God. Nevertheless, in the course of our growth to understand and know who we are, we found out that we are divided, and corrupted by religious doctrines, tribalism, nationalism, and by diverse social &political ideologies. Eliminating all these, we are the sons and daughter of the same father who can share one bread and drink one cup at the same table.”
God. Nevertheless, in the course of our growth to understand and know who we are, we found out that we are divided, and corrupted by religious doctrines, tribalism, nationalism, and by diverse social &political ideologies. Eliminating all these, we are the sons and daughter of the same father who can share one bread and drink one cup at the same table.”
“If Jesus was called by his own brothers and
sisters as "a man who was out of his mind one day" thus if you
believe in Jesus and trust him, in his name you might be also called "you
are out of your mind" by your own brothers and sisters,instead of
revenging to them say "Amen" to Jesus the Lord and he will grant you
wisdom and knowledge in abundance.”
“It's unwise to cling to the topmost step mean
while the next steps before the top most step have neither been stepped on nor
recovered. Thus in life every step/stage has got a role to play, otherwise
skipping steps in life to cling for the one that seems better is what i may
call "making short cut in life" all those who have ever attempted
life short cut to cling for the best have found themselves in a place they
wouldn't want to be. Courage, vigilance and perseverance are the only key
solutions to gain what's noble(the highest stage).”
“Don't get amused when people clap for you,
rather think twice the reason for their clap,and the reciprocal cost that has
to be paid for the clap.”
“It somehow surprises me when i think of the
fact that, money is made of papers and coins. Money can't speak, yet it makes
people to speak wisely or violantly. Money can't move because it has neither
hands nor legs, yet it makes people to move a far distances. Money is
dressless, yet it makes people either to look smart, or to look lough!
Furthermore, money makes others to look mad/crazy while they are not at all.
Though money is speechless nobody dare to fear it. What's in money is a big
deal, only God knows.”
“Mtu huitwa kichaa au mwendawazimu pindi anapopotelewa
na dhana ya aibu kabisa kwa yale ayafanyanyo mbele ya watu. Ukichaa na
uendawazimu hizi pia ni dini za pekee.”
“If you want to prove that you are really
genious think of the wonders you have done to an extent that both ordinary and
extra ordinary minds get suprised! Don't light a candle infront of blind men,
and call your self a genious man, but think of how you can make an inventory
that had never been into existence, thereby you can call your self a great
thinker of the great mind.”
“If you want to know how people hate or love
you, involve in a serious issue that's about to cost your life.”
“It's better to accomplish the assigned task,
than keep on lamenting before accomplishing it.Our daily assigned tasks however
simple or difficult they are, is God's calling to us and infact this is our
vocation to accomplish what we have been assigned to do.”
“Somebody's simplicity, humility
&humbleness is not confirmed by appearance but rather it's confirmed,
tested and judged by his/her ways of conducts (By words &deeds)”
“To be given a bottle of cocacola by somebody
you meet on the street is not both a guarantee and conclusion that he/she is a
good person! If you want to know and understand who is really a good person
have your enough time to live with him/her. At the end you will realize whether
the person is good or not. N.b. Bear also in mind that goodness /badness might
be subjective in accordance with determined circumstance of the issue in
question! Thus it's irrelevant to evaluate and give the conclusion of the
reality due to first impression without having a recourse on the entire
experience of the judged phenomena.”
Top of Form
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)