Jumanne, 20 Oktoba 2015

UMASKINI WA MALI AU UMASKINI WA FIKRA?

Inashangaza kuona watu wanambiwa na kupewa ahadi kuwa wataondolewa umaskini na kuwafanya wawe na maisha mazuri. Umaskini wanaouongelea waheshimiwa ni umaskini upi?kuna umaskini wa fikra, umaskini wa njaa, umaskini wa hela, na umaskini wa elimu,sasa waheshimiwa wakisimama kuwapigia watu tarumbeta ya kuleta mabadiliko na kuondoa umaskini mbona hawaelezei namna na jinsi watakavyo mfanya kila mtanzania aondokane na umaskini wa aina zote zilizotajwa hapo juu?inawezekana ukawafanya watu wote nchi hii wakawa kweli matajiri au ni siasa inayosukuma hayo mambo kuliko utawala wa akili na kufikiri juu ya hao waheshimiwa wayasemayo?Hata nchi zilizoendelea bado zina maskini,inakuwaje sisi Leo tuambiwe kuwa baada ya uchaguzi tunakuwa matajiri bila hata ya kuonyeshwa ishara halisi kimatendo ila kwa maneno ndo kwingi?Hayo yote ni kuongelea mdomoni kuliko kongelea akilini.

UMRI WA UZEE NA MAHITAJI YAKE

Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto

ELIMU NA UMUHIMU WAKE

Elimu ya uraia(zamani Siasa) na somo la filosofia ya siasa ni vitu mbavyo katika mapana yake katika nchi yetu havijapewa kipau mbele sana na huwa vinachukuliwa kama masomo ya ziada au nyongeza. Ukosefu wa uhelewa mpana wa mfumo wa siasa na utawala na matabaka yaliyo katika mfumo wa utawala umetufanya wengi tuwabebe walafi na wanyonyaji waliojikita tayari nyuma ya pazia la siasa wakijenga mahekalu.Tukumbuke kuwa mifumo yote tuliyonayo ya utawala haipo kwa ajili ya kumnufaisha mwananchi mwenye kipato duni Bali kujishibisha na kile kinachobaki baada ya kujishibisha kinatupwa kwenye mashimo marefu ambayo hata mlalahoi hawezi weka mkono na kukifikia(utoroshwaji WA hela za walalahoi na kufichwa nje ya nchi-Uswiz).Hao hao ndo wakishashiba wakaona uchaguzi unakaribia ndo hutumia masalia yaliyokuwa yamefichwa ngambo,hela ya haohao walalahoi waliyoisha sahau kama ni hela na jasho lao kuwalaghai wawapigie kula,hela hiyo ndo inatumika kuwanunulia hao walalahoi tishert na kofia ikiwemo kilauri ya pombe na hatimaye humpigia makofi mlafi na kuendelea kumweka madarakani;na kumfanya aendelee kuneemeka kwa kuwaibia zaidi.Maisha bora kwa kila mtanzania yanakujaje?maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwajengea watu shule za kata sisizo na miundo mbinu bora za kufanya kazi ikiwemo walimu wa kutosha, maisha bora kwa kila mtanzania ni kuwanyima baadhi ya wahitimu mikopo ya kusoma elimu yajuu wakati huohuo wale wasemao maisha bora kwa kila mtanzania watoto wao hakuna hata mmoja wao aneyesoma shule ya Kata.Au maisha bora kwa kila mtanzania ni kuona watu wanakosa huduma katika hospital za serikali hadi wanapoteza maisha wakati wale walioshikilia ile keki ya juu wakiumwa mafua wanaenda kuyatibu hayo mafua London.Hayo ndo maisha bora kwa kila mtanzania. Timefikia wakati wa kukabidhi mbuzi wetu fisi akatuchungie.Tumefika wakati wa kuchezewa viini macho na kutoa dhamana ya nchi kupitia chezo mazingaombwe unaofahamika kwa wachache ambao 

JIBADILISHE KABLA HUJABADIRISHWA

Itawezekana kupata mabadiliko ikiwa wanaodai hayo mabadiliko hata wao wenyewe hawajajiletea mabadiliko hata kwa mambo madogo waliyonayo?mfano kama mtu anadai mabadiliko wakati hata magugu yaliyozunguka nyumba yake yanamshinda kuyangoa, mtu akishindwa kufagia nyumba yake na kuipanga vizuri na hata akashindwa kupanga chumba chake anapolala mwenyewe sasa ukisikia huyo anadai mabadiliko huyo kweli anadai mabadiliko kutoka ndani ya moyo wake au ni msukumo wa mikumbo ili mradi siku imeenda?Itawezekana kweli kudai mabadiliko ihali mdai mabadiliko hajajibadilisha na kubadilika na hatimaye kudai ili abadilishwe zaidi.Kamwe haitowezekana mabadiliko kwa watu kama watu wenyewe hawajajibadilisha katika vitu vifuatavyo:1.Kujibadilisha kifkra 2.Kujibadilisha kimtizamo hasa juu ya kufikiri,kutenda, na kuchukulia uhalisia wa mambo.3.Kujenga mtizamo chanya na kujikubali mapungufu 4.Kuondoa dhana ya kujihisi wanyonge daima na hivyo kujenga dhana ya kuwa wategemezi daima. Kwa hili ni kuwa dhana ya kutegemea kila kitu kupewa ndo wengi tumejikuta tunaitwa mbumbumbu na hivyo kutengeneza mwanya kwa waheshimiwa kutoa ahadi hewa za mabadiliko yasiyokuwepo.Tusipojibadili namna ya kuchukulia na kufanya mambo tutajikuta hatuna mabadiliko kamwe.Haiwezekani ukalala bila ya kufanya lolote na hapo ukategemea mabadiliko yatokee.Kuleta mabadiliko ni moja ya mapinduzi katika historia.Tukumbuke kuwa hustoria ni kwa wale tu waitengenezayo(history is only for those who make it,never sleep and expect history to be made for you).Mabadiliko yatakuja pale ambapo tulisha anza sisi wenyewe kwa Yale madogo tuliyoanzisha kwa juhudi zetu wenyewe

LUGHA NA MATUMIZI YAKE

Matumizi ya lugha isivyo hitajika yaweza kupoteza ukweli wa mambo kihalisia na kufanya hata watu wasiohusika hata vitu visivyoweza kutumia ufahamu(reasoning) kuonekana kuwa vina hatia. Mara nyingi tumeshuhudia mfano ajali nyingi hapa kwetu na duniani kote.Ajali kama hizo zimehusisha watu kupoteza maisha kutokana na hizo ajali. Mfano tumeshuhudia ajali za vyombo vya moto kama vile pikipiki na magari, ndege,na vinginevyo. Jambo ambalo huwa daima linanishangazaga ni kwenye mawasiliano wakati wa kutoa taarifa baada ya kutokea ajali mfano utasikia mtu anaongea kuwa " nimeangushwa na pikipiki,au nimeangushwa na gari" hivi kweli hii inawezekana kimaongezi kuwa mtu ameangushwa na pikipiki au gari? mimi naona kuwa hiyo siyo sahihi kamwe.Daima mtu huwa ndo anaiangusha pikipiki au gari maana hivi vifaa vya usafiri huwa havina akili au utashi wa kuamua kumdondosha mtu bali uzembe wa mtu huwa ndo unamfanya adondoshwe au aangushwe na hicho kifaa cha usafiri.Hiyo ndo kawaida yetu binadamu kuwa huwa hatupendi kuwajibika kutokana na uzembe wetu baadala yake ni kuhamishia maumivu na hisia kwa watu na hata vitu visivyo na uhai kuhusika na mikosi tuipatayo. Nimesikia mara nyingi mtu mmoja akisema kuwa kamwe hatopanda pikipiki, nilipomuuliza sababu ya kusema vile akaniambia kuwa ni kwa kuwa pikipiki zimeangusha na kuua watu wengi;swali langu kwake lilibaki kuwa " je pikipiki huwa inaangusha mtu au mtu huwa ndo anaiangusha?" Uwajibikaji ni muhimu kabla ya kuelekeza tuhuma kwa wengine.

KWA NINI WALIMU WANAPATA UJIRA WA KUBABAISHA?

Tujiulize swali la msingi kuwa kama walimu wetu wangelikuwa wanalipwa posho kama za wabunge kwa mwezi kungelitokea nini katika sekta ya elimu?Hivi huyu anayeenda kuwakilisha wananchi katika chombo cha dola ambacho ni moja ya mihili mikuu ya serikali kimaarifa au kielimu huyu inasemwa kuwa walau awe na elimu ya kidato cha nne na zaidi ajue kusoma na kuandika basi. Cha kushangaza na kuchekesha ni kuwa huyu ambaye anasemwa kuwa ajue kusoma na kuandika mara nyingi huwa tunawaona kupitia Luninga wakiwa wamechapa usingizi na kusahau kile kilichowafanya wawe hapo;kisa ni kujua kusoma na kuandika na mwishowe huyo anapata posho Mara nne au tano ya mwalimu au mtu yeyote mtaaluma ambaye kila siku lazima asumbue kichwa chake kufanya kazi Fulani,wakati waheshimiwa wanalala na posho inaingia.Hivi ninani ambaye hawezi simama pale bungeni na kutoa hoja? kusimama pale kunahitaji kuumiza vichwa kweli?jibu ni hapana ila kukaa pale ni sawa na kusema kama waswahili wa mtaani wasemavyo"kula kuku kwa mrija." Hii itakuwa sahihi nikisema kuwa baadhi ya wataaluma wetu hasa maprofessa wetu wa vyuo vikuu wanaacha fani zao na kukimbilia kwenye siasa maana huko kuna ulaji kwa njia ya mtelemko bila ya kusumbua vichwa.Hivi kama hao wanaokimbia fani zao na kuingia katika siasa wangelikuwa wanapewa keki wanayopewa hawa waheshimiwa bungeni tungelikuwa hatua ya juu sana kielimu. Uwezo wa kujenga hoja na fikra hautegemei kusoma na kuandika,Bali unahitaji pia nguvu ya kufikiria na kujenga hoja makini.Wale waliopaswa kushauri wanaoongoza pia nao wanataka kuongoza,je hapo nani atatoa maoni na ushauri kwa wanaoongoza?matokeo yake ni kuishia katika ushabiki usiojenga

MAADILI JUU YA AHADI.

Ahadi yaweza kuleta matumaini ya kuishi kwa muda mrefu bila ya kuona ukweli wenyewe au uhalisia wa hiyo ahadi.Kwa kifupi naweza sema ahadi siyo tofauti na ndoto maana hivyo vyote ni ishara zinazolenga kwenye uhalisia japo zenyewe siyo uhalisia(reality)kamwe. Ahadi ni kama vile mtu kusikia harufu ya chakula kikipikwa au kukaangwa akasikia kushiba kumbe ihali bado ana njaa ya kutosha. Sasa wengi wetu ndo hali tuliyoifikia wakati tukielekea uchaguzi mkuu.Hivi hizi ahadi zinazotolewa na waheshimiwa tukapiga makofi kwa nguvu tukafanana na waliokwisha kula na kushiba, hivi huu ni ukweli na uhalisia au bado tuko kwenye ndoto?.Kuna namna nyingi zakudanganywa na ukakubali kiulaini bila ya manunguniko.Njia mojawapo ni ahadi ambazo ni nusu ya uhalisia na nusu uongo.

KWA NINI KUTAWALIWA NA HISIA BAADALA YA KUTAWALIWA NA UFAHAMU?

Ni jambo la kushangaza kuona watu wanatawaliwa na hisia(feelings) za wengine na kuzifanya hisia zao.Kimsingi kundi la watu wa namna hiyo linakuwa limepoteza malengo na mwelekeo kwa ujumla katika maisha.Ukiangalia ushabiki unaofanywa kwa sasa katika vyama vya siasa unaweza tambua kuwa sio mashabiki wote wanajua walitendalo ila wengi wao huenda kwa mkumbo wa kwa kuwa Fulani kashabikia hebu na Mimi nishabikie kitu ambacho ni hatari katika maendeleo na utu wa kila mmoja wetu.Hivyo hatuko mbali kusema kuwa ushabiki ninamna ya watu kuishi maisha ya wengine ili mradi siku ipite.Ushabiki lazima uwe na tija na malengo pia ya kumnufaisha mwananchi kuliko kumnufaisha mgombea.Ni heri kutoshabikia yale tusiyoyajua maana wanaofaidika ni wengine.Kwa jina la ushabiki wengine wameshanunuliwa kwa kilauri/kiloba wakiwa wamesahau kuwa wanauza utu wao na haki zao kwa vitu vya mpito visivyokumbukwa daima.

NANI AHUDUMIWE NA NANI ALALAMIKIWE?

Kama wanaohudumiwa wanawalaumu na kuwalalamikia sana wanaowahudumia, je wanaohudumia watahudumiwa na nani?na wakilalamikiwa nawao watamlalamikia nani? Siyo vema kulaumu na kulalamika kilawakati maana na hao wanaolalamikiwa wana haki ya kulalamika nao ni binadamu kama binadamu wengine.

MIFUMO NA MADHARA YAKE

Kuna wengi ambao kiutendaji huonekana wema.Tatizo linakuja pale ambapo utendaji wao unazoroteshwa na kumezwa na mfumo mama uliowalea hadi wakaota vitambi na mvi.Hao watendaji daima huishia kuumia na kuzikana nafsi zao ili waendelee kulea na kubeza mifumo iliyowalea hata kama wanaona kuna mapungufu.Wakijaribu kuinua na kupaza sauti zao wanajikuta wanalaumiwa na kulumbambana na hao wazazi wao(mifumo)iliyowalea.Mifumo ipo na inaendelea kuwepo katika jamii ili iendelee kuneemeka.Waendao tofauti na mifumo hao ndo wanaonekana kukimbilia upande mwingine wa shilingi. Pia ikumbukwe kuwa mifumo imetawala nyanja mbalimbali mbali katika jamii yetu. Wale ambao wanaonekana wema na watakatifu na wanaopaza sauti zao wakilalamikia mifumo iliyopo kwa sasa, wakishapewa nyenzo tutashuhudia mda si mrefu wao watajenga mifumo ya namna gani?either mfumo wa kujifaidisha wenyewe au mfumo kwa ajili ya manufaa ya wote?lazima tutambue kuwa binadamu ni fumbo ambalo halijafumbuliwa na lisilo rahisi kueleweka kwa kila mtu.Yule anayelia na kuwafanya wengine walie,je wale waliao wakimfikisha mliaji anapotaka je wao wakianza kulia atawasindikiza na kuwafikisha wanapotaka(wananchi)?Wanaoonekana kuomboleza wakisha fikishwa mahala pao wanapotaka daima hujenga kuta ili kuwazuia waombolezaji wasiingie pale walipofika(Ikulu).Tusikumbwe daima na mikumbo ya kutekwa na kuwa watumwa wa mifumo tusiyo ijua malengo yake.

UCHAGUZI MKUU UMETUFIKIRISHA NINI?

Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake, kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.

MCHEZO WA SIASA NI MCHEZO WA NAMNA GANI?

Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake, kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.

HUU NI WENDAWAZIMU KUPIGA BARABARA DEKI AU?

Nijambo la kutafakarisha kuona watu wanapiga barabara deki tena kwa nguvu zote! na hili kimsingi siyo jambo la kawaida hata kidogo.Waweza jiuliza nini kinawasukuma watu kufanya hivyo?je wanafanya hivyo kwa ushabiki au kufanya hivyo kunaashiria jambo Fulani? Kama tujuavyo watu wakifanya hivyo wanakuwa wanaashiria jambo fulani kwa kutarajia litokee na kuwafanya wawe katika hali fulani ya maisha. Tunajua kabisa kuwa alama zionyeshapo uendapo huwa daima zinasaidia kuonyesha mahali sahihi unapohitaji kwenda japo alama zenyewe siyo mahali unapotaka kwenda. Tukiona watu wanapiga deki na kupangusa Barabara wanakuwa hasa wanatoa ishara gani? hapo twaweza kuwa na majibu na fikra nyingi. Mojawapo ikiwa ni kwamba wamechoshwa na mfumo mbovu wa uongozi wanataka uongozi mpya na dira mpya ya maendeleo, au kwamba wananchi wanataka sasa kupumulia mahala pazuri pasipo hila wala uyanganyi wala ufisadi n.k hayo ni baadhi ya majibu waliyonayo wapiga kura.Kiuhalisia siyo jambo la kufikirika watu kutumia mda wao mwingi kusafisha barabara pasipo kuambiwa kufanya hivyo au pasipo malipo isipokuwa kuna jambo fulani ambalo kwa wasio funguka macho bado ni kitendawili.

MTU NA UTU WAKE

Ukitaka kutambua utu wa mtu na kumjua yeye ninani mpe Uhuru wa umfanyie nini?hapo ni dhahiri kuwa utapata majibu mengi kutoka kwa huyo mtu juu ya analotaka umfanyie hata kama mengine yapo juu ya uwezo wake.Katika nafasi hiyo utapata kutambua kama huyo mtu ni mchoyo na pia mwenye uchu wa kutaka kutawala au pia utapata kujua unyenyekevu wa huyo mtu kadiri ya kitu ambacho amekuomba ukamfanyie.Sasa tuje ngambo nyingine ya Shilingi ambapo Leo hii tumeshuhudia wale waliokuja kutuomba dhamana ya kuongoza nchi.Wao wakati wanahangaika ili tuwape dhamana ya kutuongoza mambo yamekuwa kama ifuatavyo:1.Wao wamekuja na bado wanazidi kuja kwetu na tumewauliza "je mwataka tuwafanyie nini?" Wao wakajibu kwa sauti kubwa "mtupigie kura ya ndiyo katika uchaguzi mkuu ujao."2.Pindi na sisi ilipokuwa zamu yetu juu ya wao watufanyie nini, wamekuja na majibu mbalimbali yenye kutia moyo japo hayana uhakika asilimia mia moja.Moja ya majibu mepesimepesi ni kufuta baadhi ya Kodi, Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.Kuanzisha viwanda, kuhakikisha kuwa vijana wote(waliosoma na wasiosoma)wanapata ajira na wanakuwa na maisha mazuri n.k.Hayo yote ni mazuri sana ila wengi wetu tunasahau kuwa siyo kila ahadi utekelezeka! Kwa Mawazo yangu ni kuwa itakuwa rahisi kwetu kutoa majibu ya maswali yetu ya tuwafanyie nini waheshimiwa maana majibu yanaeleweka, kuwa tutawapigia kura ya ndiyo.Wasiwasi unakuja kwa majibu ya maswali yetu kwao kuwa watatufanyia nini?majibu yao kwetu yamekuja na ahadi ambazo ni vigumu kuamini kuwa zitatekelezeka.Tunasahau kuwa Siasa ni mchezo ambao siyo wote twaweza kuucheza. Punde tutashuhudia kama tulidanganywa juu ya hizo ahadi au la! wakishapewa hayo majukumu ndoo itakuwa kutekeleza au kutokuteleza hizo ahadi.Hofu yangu ni kwamba kwa nchi kama Tanzania,Ahadi zilizotolewa baadhi ziko nje ya uwezo wake, kama vile Elimu bure na ajira kwa kila mtanzania hasa vijana.Hayo yote ni majibu ya tutafanyiwa nini.Yatubidi tufunguke macho na kuelewa kati ya kuambiwa ukweli au kulaghaiwa.

LUGHA YA BAO LA MKONO

Kwa sasa tunaambiwa lugha ya bao la mkono! bao la mkono halikulezewa vizuri na kuzungumzika vizuri.Mtoa hoja angelielezea vizuri ni mchezo gani ambapo bao la mkono ni marufuku mfano katika kucheza mpira wa miguu ukifunga bao la mkono jua kuwa kuna adhabu juu yake(Penalty) wakati kama unacheza Mpira wa mikono(volleyball au Basketball) gori la mkono hapo hapo halina shida. Shida ni pale bao la mkono linafungwa wakati wa mchezo wa mpira wa kutumia miguu.Afungaye kutumia mkono kwa mchezo wa Mpira wa miguu hapo inamhitaji abadilike. Katika mfumo wetu wa utawala yaonekana wananchi wameumizwa vibaya na kufikiria vinginevyo kwamba mabao yanayofungwa siyo halali kwa kuwa mchezo unaochezwa ni mchezo wa mpira wa miguu lakini bado mabao yanayofungwa ni ya mkono pasipo halali(utumiaji wa nguvu kupita kiasi na rushwa).Bao la mkono litatambulika kuwa hivyo na halali pindi mchezo ukiwa wa kuchezwa kwa mikono na siyo miguu.Kama wananchi wanalalamikia bao la mkono hii inamaana gani? kwamba mchezo unaochezwa ni wa miguu ambao kiutaratibu lazima bao kama bao linafungwa kwa miguu,Ila matokeo yake washangiliaji wanaona bao linafungwa kwa mkono wanashangaa na kufikiri kutowezekana kwa hilo bao lililofungwa na wakati huo refaree anaweka tiki kuwa ni bao stahiki mbali ya kujuakuwa siyo halali.Tujiulize kuwa katika uwanja wa Siasa wachezaji wanacheza mchezo gani? wa kukubali mshindi halali au lile bao la mkono?

Ijumaa, 29 Mei 2015

WHY TO RISK FOR NO APPARENT REASON?

"Never be separated and torn apart by people's differences whose source is not your concern"

Ijumaa, 22 Mei 2015

THE FALL OF A BIG MAN

"The fall of honourable person in the society  is always accompanied by a big bang"

FR. REVOCATUS PAUL'S QUOTATIONS

“In a moment when truth is being derivered to those who have been deprived of it, on their part it becomes a joyous moment but on the contrary when the same truth is delivered to the counterpart it becomes a bitter moment,Yet the same truth once not accepted it makes a step a head of the one who has rejected to embrace it. Accepting a truth is not instantenous process, it is a gradual process.In one way or another no body here on Earth has dared to embrace the absolute truth.What majority embrace is that which seem to be equivalent to truth.However truth with time should be embraced either in calm moments/displeasurablemoments.Those who have mismanaged truth I dare to call them liers.

“Money is a decorated house for the devil.The devil welcomes those who abuse the use of that commodity called money into his decorated house.Thus money is the hidden trapof a devil waiting to catch those who mismanage it.”

“You can't climb the ladder of achievement while hands are on your pockets” (C.Niger)
“Lawless society/community will result into powerless against powerful individuals.The voice of the voiceless will never penetrate the voice of powerful individuals in a lawless society.Those in power are becoming ambitious to alter the constitutions of their respective countries to ensure that they remain in power for ever.Such people tend to think that they were born alpha and omega presidents.In Africa majority of our countries are ruled under the umbrella of democracy while in real sense what is happening at the ground is a drama of surviving for fittest vs weak people. What's really at stake in African politics is the gymnastic competition of those having strong teeth to tear aflesh against toothless individuals, honestly speaking who will win the competition?definitely are the ones having strong teeth to tear flesh on their predators(citizens).Our Leaders unlawful become presidents under Machiavel's principles(The end does not justify the means-If you want to be a leader make sure that you become,e.g if it's through shedding blood of Innocent people that is not a problem what matters is for an individual to become a leader).Let's pray for our dear brothers and sisters who are tormented by such system of Political ruling system without excluding Burundi,Zimbabwe,Uganda to mention but few.”


“Giving out of charity is moral and religious obligation on the part of the donor,but on the part of the recipient is not obligation, the constant charity donation to the recipient on the other hand turns out to be mandatory on the part of the donor.The recipient because of constant receiving charity from the donor turns it out to be obligation even if the donor has nothing to give yet the recipient will keep on demanding to be given even what is not there. When a recipient has not tested how to have what is given is found he/she won't stop demanding much.In order to let the recipient who has been given charity freely test how it is found never give him/her fish, rather teach him/her how to fish.
“It's good to hear people's advices,yet it is dangerous to be at people's disposal,once you accept that condition of being at one's disposal it means you are owned as any other property,you are no longer free to express the freedom of your conscience. Being at peoples disposal is slavery created unknowingly/knowingly. Because of poverty majority have found themselves victims of being owned like any other property while in real sense they are both conscience and thinking beings(rational animals)

“It is surprising that we have what we call university Lecturers,Doctors,and Professors, some of these academicians have been given these academic titles undeservedly.If you have done tertiary(university education) It's my hope that you have realized that some of the mentioned people above hold academic credentials they are not supposed to hold. The cause of this is due to fact that in their teaching and presenting materials to their students they seem to be not what they hold as their academic status. Poor presentation of staff to the students is an indication that a Professor/Lecturer/Doctor was not qualified to that title because of the following reasons:1.In the course of his study he/studied the course by claiming and memorizing without understanding the core subject at hand. 2.Plagiarism:In this fact majority falls to this category,this concerns those who copy other peoples works and acknowledge them as their original work.Some even have dared to copy and paste peoples thesis and dissertations and thus acknowledge them as their original work for academic credit.This is what we call an intellectual theft! down the centuries these people have been there and are still there eating where they have not sown.This to say is not different from other graft public scandals.Academic irregularities and dishonest is a big scandal beyond corruption scandal.Our government is silent on such people being in our universities and public offices holding the titles they do not in fact deserve. The government should be courageous to take the disciplinary measures against these people.Yet the challenge ahead is that who will fix the bell at cat's neck??those holding high public offices are the one in front line being victims of academic irregularities and dishonest! who is able to confront the other? Corruption has become an incurable disease that is eating our institutions?will PCCB be able to deal with these intellectual robbers in our universities and public offices?”
“Wahubiri siyo kazi yenu kuhubiria waumini wenu na kisha kuwaacha mawinguni Bali wahubirieni hadi mkawafikishe mbinguni(Polepole kwenye semina ya kura ya maoni ya Katiba pendekezwa jumbo kuu Katoliki la Arusha)
"A good speach is motivated by prior preparation of an occassion to be discussed."
“It's useless and silly to be critical on other affairs that won't benefit you at all.Critical minds are the one's that seek to construct and not to destroy what has been already constructed. If you can't construct never attempt to destroy ready made reality /thought

“The use of mobile phones has facilitated many things to be done in a short period of time.This has made communication to be easy as we can imagine.The use of this technology has somehow to a greater extent replaced the local method of communication like postage communication, and Landline telephone communication system.All in all we have the courage to thank God for having enlightened the scientists mind to discover such an easy communication facility.However,there has been shortcomings due to use of this communication technology,to mention few examples,it has been found that the use of mobile technology in facilitating communication also has resulted into cyber crimes like theft, the use of this technology has also resulted into illegal marital affairs (breaking of marriage),it has resulted also into psychological in equilibrium due to mismanagement of the communication facilities.There are many things that have to be discussed concerning the abuse use of the communication facilities.”
“When being invited by your relative/friend to an ocassion never refuse to attend that event, the event may once change your way of thinking and your way of looking at things. Availing at an occasion does not necessarily mean to eat and drink,but it also mean meeting people and exchange World's view and life reality.through this process,thus when you attend an occasion it is also a chance for personal transformation and maturity.
“Kwenye jamii hawakosekanagi watu wa kulaumu wengine hata wakikosa wa kulaumu basi wao hulaumu kuwa kwa nini waliumbwa? Watu kama hao ndo waitwao wale watafutao ukamilifu na mambo yote kwao huwa wanataka yawe makamilifu(Perfectionist people) hawa huwa hawakubali mapungufu ya wenzao ila huwa wanapenda ukamilifu kwa wengine.Hivyo kundi hili la watu wapendao kuona ukamilifu(perfection in others) wanakuwa siyo rahisi kuishi na kuelewana na jamaa na rafiki zao.Ni kwa msingi huu tunaona kuwa watu wa namna hii siyo rahisi kuwa na marafiki wengi kwa kuwa wao huona kila mtu siyo mkamilifu kama wao watakavyo.lawama na kuwalaumu wengine kuwa wamekosea bila hata kuangalia mazuri yao huwa kwa wakati mwingine inamfanya huyu apendaye ukamilifu kwake na kwa wengine daima aishi ulimwengu wake aujuaye yeye. Na kwa kutengeneza ulimwengu aujuaye huyo atakaye ukamilifu si ajabu wale wasio wakamilifu oia nayeye wakaona mapungufu yake na hivyo kupelekea kuitwa mwenye akili sana au mwendawazimu. Heshima kwa utu wa mtu yakiwemo mazuri na mapungufu ya mtu huwa ndo vinajenga utu wa mtu.Vile avifanyavyo mwanadamu huwa ndo vinajenga na kubomoa utu wake.Utu wa mtu kwa ujumla ukamilishwa na mahitaji yake ,mazingira,na oia watu aishio nao. Mtu asiposifiwa kwa yale ayafanyayo utu wake unakuwa umefananishwa na yule mtu aonaye dhahabu iliyochanganyikana na matope akaamua kuitupilia jalalani baadala ya kuondoa tope ns kuchukua dhahabu. Vivyo hivyo mtu akiwa na mapungufu siyo kuwa ni mbaya,upande mwingune wa Shilingi ni kuwa mtu huyo mabaya yake yakiondolewa bado anamazuri ya kunufaisha jamii.Hivi ni wangapi wametupwa majalalani na mazuri yao wakidhaniwa kuwa ni wabaya wakutupwa???Tutafakari juu ya hilo.”

“Ukikutana na yule usiyemjua njiani usimcheke/kumdharau/kumsengenya kwa namna alivyo kwa kuwa huyu aweza akawa anaenda nyumbani kwako na pia aweza kuwa mtu mashuhuri ambaye siku zote umekuwa ukisikia habari zake na pia ungelipenda kukutana naye siku moja.Kumbuka kuwa cheo cha mtu huwa hakimbadilishi sura,ila watu wamjuaye huyo mtu huwa ndo wanampaka sura kutokana na cheo chake na matendo yake kwenye jamii aishiyo.”

“Don't look at rich people and think that they became rich within a day, their state of being rich has left the history behind! If you attempt to examine, and analyse their history of how they got there, somehow the nature by itself will tell you a lot concerning Histories of such rich men, which include good and bad histories.All in all History remains a history despite of its good/bad attributes.History is for those who make it.

“If you want to know who is a real friend to you, just mention your problem to him/her.From his/reaction it's when you will notice his/her concern to you.”

“Binadamu daima huwa hakosi kisingizio.Akikosa kumsngizia mwanadamu mwenzake basi atasingizia utupu,giza na mwanga.”



“A man who said to have been a university graduant was some where looking for an employment, thanks be to God in his going around he saw an advatisement inviting candidates of his qualifications to appy for a job on that particular company, a man being delighted went with his credentials ready for an interview, reaching at the gate of the company he found a very simple and short Man standing at the gate talking to a Watchman, when a man being asked what was he looking at the Company a man unhestatingly replied" I want to meet a boss of this Company, I am having an issue with him" the simple and short Man at the gate asked him " which issue are you having with him?" A man replied, " sorry it does not concern you, please tell me if the boss is around or he is not around? and don't waste my time". As the interogation was going on between the university graduant looking for a job in the company, and the short Man, thus a confrotation between the two arose. At the end of long argument and confrotation, the short and simple man revealed himself that he was the company's boss. He told a university graduant that he had already failed an interview! Lesson. Pay respect to people you meet because you never know that when you are looking for something they are the ones to find that thing for you. Being wise and prudent in dealing with others is passmark for our daily interviews.”

“Everybody who is idle, potentially is the green pasture where the devil may be fed on.”

“When people don't speak something about you, don't think that they don't know you, your way of life(Moral conducts) will reveal to people who are you, this qualifies people either to talk good things about you or to talk evil things about you. Nevertheless, the challenge here is that majority prefer to speak scandalous news about others instead of good news! what pushes them to act like that? It's because the devil has been at work and is at work to ensure that good minds are corrupted in a way that they can't see goodness on others.

“The way you are( Physical make up, Psychological make up, mental make up, social make up) is the way God wants to communicate to others and make them learn from you. Don't disapprove God for having created you the way you are, He has got purpose to create you,the plan of God to our life is beyond our intellectual grasp. Let God fulfill His plans and Purposes in our life. Remember that Comparison in life breeds contempt. God has created every body in a unique way in order to accomplish the design of His creation.”

“Human beings are only beings but are beings after the attention and understanding of meaning in life.”

“Evil men should not be blamed for corruting the World,rather those who have to be blamed are those people keeping quite amidist of evil men without any discplinary action thus creating an evironment for evil doers to flourish.

“Society without regulations& laws is like life in a zoo.”

“Food for thought: Just think ten years ago had you ever thought to be where you are and do what you are doing now? have you ever thought what will you be doing at the time like now for the next ten years to come? if the answer is Yes,then how do you know it? If the answer is no,then submit your hopes&expectations into the hands of God.

“The truth said by our elders to avoid a certain ways of conduct can't be accepted instantly. The truth foreseen by our elders never fade away, it rather proceeds a head, extra mile. It awaits to reveal by itself when the circumstance foretold by the elders to be avoided reoccurs. The truth is ever a head of Man's thinking. Let a truth be a truth. A lie will never complement a truth.

“What makes people to love or to hate one another is not one's physical make up, rather it's one's bodly languages and ways of conduct. By nature man is born good, nevertheless,after being brought fourth in a society, thus he/she becomes corrupted by societal influences.

“In order to know man's humbleness and responsibleness , two prerequisites are need .1. Let him/her be left free to do whatever he/she likes 2. Let him/her be given a mandate to exercise his/her freedom on others.”

“Two brick's makers were found making bricks when were asked what were they doing one replied"I am building a cathedral, the other replied "I am mixing sand and cement to make bricks, between the two who gave a correct answer?

“Kuna bwana mmoja ambaye ukimwangalia kutoka kwa mbali alikuwa anapendeza
sana, ila ukimkaribia kidogo sura yake na maumbile kidogo vilikuwa vya kutatanisha. Kope za macho yake ni kama za mbuzi, ndevu kama mashurubu ya paka, mwili wake mzima ulijaa manyoya na vitu vingine vingi. FUNDISHO. Ukitaka kumjua mtu ninini na ninani usiishie kumtazama kwa mara moja ila kaa naye na uishi naye hapo utaona mengi na kujua mengi kutoka kwake bila ya kuacha mashurubu ya
paka nyuma.”

“Naturally we are all born free,and uncorrupt. We are all sons and daughters of the same Father,
God. Nevertheless, in the course of our growth to understand and know who we are, we found out that we are divided, and corrupted by religious doctrines, tribalism, nationalism, and by diverse social &political ideologies. Eliminating all these, we are the sons and daughter of the same father who can share one bread and drink one cup at the same table.”

“If Jesus was called by his own brothers and sisters as "a man who was out of his mind one day" thus if you believe in Jesus and trust him, in his name you might be also called "you are out of your mind" by your own brothers and sisters,instead of revenging to them say "Amen" to Jesus the Lord and he will grant you wisdom and knowledge in abundance.”

“It's unwise to cling to the topmost step mean while the next steps before the top most step have neither been stepped on nor recovered. Thus in life every step/stage has got a role to play, otherwise skipping steps in life to cling for the one that seems better is what i may call "making short cut in life" all those who have ever attempted life short cut to cling for the best have found themselves in a place they wouldn't want to be. Courage, vigilance and perseverance are the only key solutions to gain what's noble(the highest stage).”

“Don't get amused when people clap for you, rather think twice the reason for their clap,and the reciprocal cost that has to be paid for the clap.”

“It somehow surprises me when i think of the fact that, money is made of papers and coins. Money can't speak, yet it makes people to speak wisely or violantly. Money can't move because it has neither hands nor legs, yet it makes people to move a far distances. Money is dressless, yet it makes people either to look smart, or to look lough! Furthermore, money makes others to look mad/crazy while they are not at all. Though money is speechless nobody dare to fear it. What's in money is a big deal, only God knows.

“Mtu huitwa kichaa au mwendawazimu pindi anapopotelewa na dhana ya aibu kabisa kwa yale ayafanyanyo mbele ya watu. Ukichaa na uendawazimu hizi pia ni dini za pekee.”
“If you want to prove that you are really genious think of the wonders you have done to an extent that both ordinary and extra ordinary minds get suprised! Don't light a candle infront of blind men, and call your self a genious man, but think of how you can make an inventory that had never been into existence, thereby you can call your self a great thinker of the great mind.

“If you want to know how people hate or love you, involve in a serious issue that's about to cost your life.

“It's better to accomplish the assigned task, than keep on lamenting before accomplishing it.Our daily assigned tasks however simple or difficult they are, is God's calling to us and infact this is our vocation to accomplish what we have been assigned to do.

“Somebody's simplicity, humility &humbleness is not confirmed by appearance but rather it's confirmed, tested and judged by his/her ways of conducts (By words &deeds)

“To be given a bottle of cocacola by somebody you meet on the street is not both a guarantee and conclusion that he/she is a good person! If you want to know and understand who is really a good person have your enough time to live with him/her. At the end you will realize whether the person is good or not. N.b. Bear also in mind that goodness /badness might be subjective in accordance with determined circumstance of the issue in question! Thus it's irrelevant to evaluate and give the conclusion of the reality due to first impression without having a recourse on the entire experience of the judged phenomena.


Top of Form




THE MIND

"The mind of a child is like a sponge ready to absolve every thing"