Jumanne, 20 Oktoba 2015

HUU NI WENDAWAZIMU KUPIGA BARABARA DEKI AU?

Nijambo la kutafakarisha kuona watu wanapiga barabara deki tena kwa nguvu zote! na hili kimsingi siyo jambo la kawaida hata kidogo.Waweza jiuliza nini kinawasukuma watu kufanya hivyo?je wanafanya hivyo kwa ushabiki au kufanya hivyo kunaashiria jambo Fulani? Kama tujuavyo watu wakifanya hivyo wanakuwa wanaashiria jambo fulani kwa kutarajia litokee na kuwafanya wawe katika hali fulani ya maisha. Tunajua kabisa kuwa alama zionyeshapo uendapo huwa daima zinasaidia kuonyesha mahali sahihi unapohitaji kwenda japo alama zenyewe siyo mahali unapotaka kwenda. Tukiona watu wanapiga deki na kupangusa Barabara wanakuwa hasa wanatoa ishara gani? hapo twaweza kuwa na majibu na fikra nyingi. Mojawapo ikiwa ni kwamba wamechoshwa na mfumo mbovu wa uongozi wanataka uongozi mpya na dira mpya ya maendeleo, au kwamba wananchi wanataka sasa kupumulia mahala pazuri pasipo hila wala uyanganyi wala ufisadi n.k hayo ni baadhi ya majibu waliyonayo wapiga kura.Kiuhalisia siyo jambo la kufikirika watu kutumia mda wao mwingi kusafisha barabara pasipo kuambiwa kufanya hivyo au pasipo malipo isipokuwa kuna jambo fulani ambalo kwa wasio funguka macho bado ni kitendawili.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni