Nijambo la kutafakarisha kuona watu wanapiga barabara deki tena kwa
nguvu zote! na hili kimsingi siyo jambo la kawaida hata kidogo.Waweza
jiuliza nini kinawasukuma watu kufanya hivyo?je wanafanya hivyo kwa
ushabiki au kufanya hivyo kunaashiria jambo Fulani? Kama tujuavyo watu
wakifanya hivyo wanakuwa wanaashiria jambo fulani kwa kutarajia litokee
na kuwafanya wawe katika hali fulani ya maisha. Tunajua kabisa kuwa
alama zionyeshapo uendapo huwa daima zinasaidia kuonyesha mahali
sahihi unapohitaji kwenda japo alama zenyewe siyo mahali unapotaka
kwenda. Tukiona watu wanapiga deki na kupangusa Barabara wanakuwa hasa
wanatoa ishara gani? hapo twaweza kuwa na majibu na fikra nyingi.
Mojawapo ikiwa ni kwamba wamechoshwa na mfumo mbovu wa uongozi wanataka
uongozi mpya na dira mpya ya maendeleo, au kwamba wananchi wanataka sasa
kupumulia mahala pazuri pasipo hila wala uyanganyi wala ufisadi n.k
hayo ni baadhi ya majibu waliyonayo wapiga kura.Kiuhalisia siyo jambo la
kufikirika watu kutumia mda wao mwingi kusafisha barabara pasipo
kuambiwa kufanya hivyo au pasipo malipo isipokuwa kuna jambo fulani
ambalo kwa wasio funguka macho bado ni kitendawili.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni