Jumanne, 20 Oktoba 2015

UMRI WA UZEE NA MAHITAJI YAKE

Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni