Mtu akifikia umri wa uzee anakuwa kama mtoto mdogo. Usione daima mzee
anakusumbua na kukuambia mambo ambayo unayaona ni ya kitoto, Bali ndo
asili ya binadamu.Ukiona hivyo msikilize kwa makini Huyo mzee awe Baba
au Mama na mpe analohitaji maana na yeye alikuwa kijana kama wewe na
hakuomba awe mzee ila ni kwa sababu ya asili ya binadamu kuwa hivyo.Na
wewe pia utafika wakati utakuwa kama huyo mzee.Endelea kushukuru Mungu
kwa zawadi ya hao wazazi wazee, usiwaone kama msalaba Bali waone kama
msalaba unaopendwa na wenye kubebeka.Maisha ni kubadilishana,ulipokuwa
mtoto wao walikuwa vijana wakakutafutia mahitaji namalezi mazuri na wewe
pia kama kijana watengenezee wazee wako mahitaji mazuri pindi
wanapozeeka na kuonyesha hali ya utoto
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni