Jumanne, 20 Oktoba 2015

LUGHA NA MATUMIZI YAKE

Matumizi ya lugha isivyo hitajika yaweza kupoteza ukweli wa mambo kihalisia na kufanya hata watu wasiohusika hata vitu visivyoweza kutumia ufahamu(reasoning) kuonekana kuwa vina hatia. Mara nyingi tumeshuhudia mfano ajali nyingi hapa kwetu na duniani kote.Ajali kama hizo zimehusisha watu kupoteza maisha kutokana na hizo ajali. Mfano tumeshuhudia ajali za vyombo vya moto kama vile pikipiki na magari, ndege,na vinginevyo. Jambo ambalo huwa daima linanishangazaga ni kwenye mawasiliano wakati wa kutoa taarifa baada ya kutokea ajali mfano utasikia mtu anaongea kuwa " nimeangushwa na pikipiki,au nimeangushwa na gari" hivi kweli hii inawezekana kimaongezi kuwa mtu ameangushwa na pikipiki au gari? mimi naona kuwa hiyo siyo sahihi kamwe.Daima mtu huwa ndo anaiangusha pikipiki au gari maana hivi vifaa vya usafiri huwa havina akili au utashi wa kuamua kumdondosha mtu bali uzembe wa mtu huwa ndo unamfanya adondoshwe au aangushwe na hicho kifaa cha usafiri.Hiyo ndo kawaida yetu binadamu kuwa huwa hatupendi kuwajibika kutokana na uzembe wetu baadala yake ni kuhamishia maumivu na hisia kwa watu na hata vitu visivyo na uhai kuhusika na mikosi tuipatayo. Nimesikia mara nyingi mtu mmoja akisema kuwa kamwe hatopanda pikipiki, nilipomuuliza sababu ya kusema vile akaniambia kuwa ni kwa kuwa pikipiki zimeangusha na kuua watu wengi;swali langu kwake lilibaki kuwa " je pikipiki huwa inaangusha mtu au mtu huwa ndo anaiangusha?" Uwajibikaji ni muhimu kabla ya kuelekeza tuhuma kwa wengine.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni