Jumanne, 20 Oktoba 2015

MTU NA UTU WAKE

Ukitaka kutambua utu wa mtu na kumjua yeye ninani mpe Uhuru wa umfanyie nini?hapo ni dhahiri kuwa utapata majibu mengi kutoka kwa huyo mtu juu ya analotaka umfanyie hata kama mengine yapo juu ya uwezo wake.Katika nafasi hiyo utapata kutambua kama huyo mtu ni mchoyo na pia mwenye uchu wa kutaka kutawala au pia utapata kujua unyenyekevu wa huyo mtu kadiri ya kitu ambacho amekuomba ukamfanyie.Sasa tuje ngambo nyingine ya Shilingi ambapo Leo hii tumeshuhudia wale waliokuja kutuomba dhamana ya kuongoza nchi.Wao wakati wanahangaika ili tuwape dhamana ya kutuongoza mambo yamekuwa kama ifuatavyo:1.Wao wamekuja na bado wanazidi kuja kwetu na tumewauliza "je mwataka tuwafanyie nini?" Wao wakajibu kwa sauti kubwa "mtupigie kura ya ndiyo katika uchaguzi mkuu ujao."2.Pindi na sisi ilipokuwa zamu yetu juu ya wao watufanyie nini, wamekuja na majibu mbalimbali yenye kutia moyo japo hayana uhakika asilimia mia moja.Moja ya majibu mepesimepesi ni kufuta baadhi ya Kodi, Elimu bure kuanzia darasa la kwanza hadi chuo kikuu.Kuanzisha viwanda, kuhakikisha kuwa vijana wote(waliosoma na wasiosoma)wanapata ajira na wanakuwa na maisha mazuri n.k.Hayo yote ni mazuri sana ila wengi wetu tunasahau kuwa siyo kila ahadi utekelezeka! Kwa Mawazo yangu ni kuwa itakuwa rahisi kwetu kutoa majibu ya maswali yetu ya tuwafanyie nini waheshimiwa maana majibu yanaeleweka, kuwa tutawapigia kura ya ndiyo.Wasiwasi unakuja kwa majibu ya maswali yetu kwao kuwa watatufanyia nini?majibu yao kwetu yamekuja na ahadi ambazo ni vigumu kuamini kuwa zitatekelezeka.Tunasahau kuwa Siasa ni mchezo ambao siyo wote twaweza kuucheza. Punde tutashuhudia kama tulidanganywa juu ya hizo ahadi au la! wakishapewa hayo majukumu ndoo itakuwa kutekeleza au kutokuteleza hizo ahadi.Hofu yangu ni kwamba kwa nchi kama Tanzania,Ahadi zilizotolewa baadhi ziko nje ya uwezo wake, kama vile Elimu bure na ajira kwa kila mtanzania hasa vijana.Hayo yote ni majibu ya tutafanyiwa nini.Yatubidi tufunguke macho na kuelewa kati ya kuambiwa ukweli au kulaghaiwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni