Jumanne, 20 Oktoba 2015

MCHEZO WA SIASA NI MCHEZO WA NAMNA GANI?

Tunavyokaribia kufanya uchaguzi mkuu baadhi ya mambo yanajitokeza ambapo kabla ya hapo mambo hayo yalikuwa hayajajitokeza japo yalikuwepo kiukimyakimya.Mfano ahadi lukuki zilikuwa hazizungumziki na hao waheshimiwa, kwa kipindi hiki cha uchaguzi ni kipindi ambapo wapiga ramli wanavuna vya kutosha.Nikipindi ambapo ikiwezekana wachawi watagundulika.Tukiendelea zaidi tunaona kuwa kila mmoja anamlaumu mwingine kwa kutokutimiza wajibu wake.Hivi katika kulaumiana ninani alaumiwe?yule aliyepewa dhamana na chama chake awe mtendaji wa serikali au chama chenyewe?Imezoeleka kusikika chama Fulani kinalaumiwa kwa utendaji,je ni halali kulaumu chama au watendaji wake?Maana kikilaumiwa chama maana yake ni kuwa wanalaumiwa wanachama wote kuanzia ngazi ya kitongoji hadi taifa kwa ujumla wake, kuna uhalali gani wa kumlaumu mwanachama asiyejua nini linatendeka na ni mipango gani inaendelea kwenye chama chake? Kwa msingi huo tunaona wengi wa wapiga campaign wakiwania ile keki nzito hutumia nafasi hiyo kulaumu chama na wanachamawake wote baadala ya kuelekeza tuhuma kwa watendaji.Mbegu hiyo hupandikizwa kwa watu nao watu huamini kuwa chama ni kibaya.Huo ni mchezo wa siasa ambao hutumika kuwafanya wananchi waamini visivyo.Mchezo wa siasa ni mchezo daima ambao wengi huuita kuchafuana(mchezo mchafu).Hivyo kuchafuana katika siasa huwa kunajumisha kuwachafua wote bila ya kuangalia ninani mhusika zaidi ya wote katika kundi.Katika lugha na maongezi ya kifalsafa na lugha ya kifalsafa kuongea kwa ufahamu wa namna hiyo(reasoning) huitwa "Fallacy of generalization),yaani kuacha kuongelea jambo husika au mhusika na baadala yake wanashambuliwa hata wasiohusika kamwe.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni